中国国际广播电台
China ni nchi kubwa yenye
mito na milima mizuri, na
utamaduni adhimu. China ina
makabila mengi yenye mila
na desturi tofauti na inajulikana
sana duniani kwa uzalishaji
wa mazao ya jadi na asilia
pamoja na mapishi mazuri ya
chakula ya aina mbalimbali.
China ina rasilimali nyingi
za utalii na uwezo mkubwa
wa shughuli za utalii katika
siku za baadaye. Pamoja na
maendeleo ya uchumi wa China
na kutekelezwa kwa sera za
kufungua mlango, sekta ya
utalii imekuwa ni yenye ongezeko
jipya la maendeleo ya uchumi.
Hivi sasa sehemu zenye mandhari
nzuri za utalii zinaongezeka
kwa mfululizo katika sehemu
mbalimbali za China, ambapo
idadi ya watalii wanaotembelea
China kutoka nchi za nje inazidi
kuongezeka kutokana na kuboreshwa
kwa miundo-mbinu nchini China.
China ni moja ya nchi ambazo
ni asili ya ustaarabu duniani,
historia na utamaduni adhimu,
vitu ambavyo vimekuwa rasilimali
yenye thamani kubwa ya utalii.
Miongoni mwa mabaki mengi
maarufu ya kihistoria nchini
China, pango kubwa la sanamu
za askari na gari la kukokotwa
na farasi la shaba lililoko
karibu na kaburi la mfalme
wa kale wa enzi ya Qing vinasifiwa
kuwa ni moja ya maajabu nane
duniani, na kuvutia watalii
zaidi ya milioni moja kwa
mwaka. Mbali na hayo, picha
za kutani ndani ya mapango
ya Mogao, mjini Denghuang
zinachukuliwa kuwa ni sanaa
adimu ya dunia. Ukuta mkuu
wenye urefu wa kilomita elfu
5 ni kitu ambacho watalii
wanatarajia kukiona kila wanapofika
China. Aidha China ina makabila
56 yenye historia, utamaduni,
mila na desturi maalumu pia
vinawavutia sana watalii.
|