RASILIMALI ZA UTALII

中国国际广播电台

      

China ni nchi kubwa yenye mito na milima mizuri, na utamaduni adhimu. China ina makabila mengi yenye mila na desturi tofauti na inajulikana sana duniani kwa uzalishaji wa mazao ya jadi na asilia pamoja na mapishi mazuri ya chakula ya aina mbalimbali. China ina rasilimali nyingi za utalii na uwezo mkubwa wa shughuli za utalii katika siku za baadaye. Pamoja na maendeleo ya uchumi wa China na kutekelezwa kwa sera za kufungua mlango, sekta ya utalii imekuwa ni yenye ongezeko jipya la maendeleo ya uchumi. Hivi sasa sehemu zenye mandhari nzuri za utalii zinaongezeka kwa mfululizo katika sehemu mbalimbali za China, ambapo idadi ya watalii wanaotembelea China kutoka nchi za nje inazidi kuongezeka kutokana na kuboreshwa kwa miundo-mbinu nchini China.

China ni moja ya nchi ambazo ni asili ya ustaarabu duniani, historia na utamaduni adhimu, vitu ambavyo vimekuwa rasilimali yenye thamani kubwa ya utalii.
Miongoni mwa mabaki mengi maarufu ya kihistoria nchini China, pango kubwa la sanamu za askari na gari la kukokotwa na farasi la shaba lililoko karibu na kaburi la mfalme wa kale wa enzi ya Qing vinasifiwa kuwa ni moja ya maajabu nane duniani, na kuvutia watalii zaidi ya milioni moja kwa mwaka. Mbali na hayo, picha za kutani ndani ya mapango ya Mogao, mjini Denghuang zinachukuliwa kuwa ni sanaa adimu ya dunia. Ukuta mkuu wenye urefu wa kilomita elfu 5 ni kitu ambacho watalii wanatarajia kukiona kila wanapofika China. Aidha China ina makabila 56 yenye historia, utamaduni, mila na desturi maalumu pia vinawavutia sana watalii.