MIJI MAARUFU YA UTALII NCHINI CHINA

中国国际广播电台

      
China ni nchi kubwa yenye makabila mengi, ujenzi wa miji ya sehemu mbalimbali Una umaalumu wake. Katika sehemu ya kaskazini ya China kuna mji mkuu wa Beijing; sehemu ya mashariki kuna Shanghai, kitovu cha uchumi wa China; sehemu ya magharibi kuna mji wa LahSa wenye umaalumu wa kitibet; sehemu ya kusini kuna mji wa Kunming ambao hali ya hewa katika majira yote manne ya mwaka ni kama ya Spring. Miji mizuri iliyoendelea ni kama lulu zinazomeremeta katika ardhi ya China yenye kilomita za mraba milioni 9.6.
Hivi Sasa nchini China kuna miji 137 iliyothibitishwa kuwa miji bora ya utalii ikiwa ni pamoja na Shanghai, Beijing, Tianjin, Chongqing, Shenzhen, Hangzhou, Dalian, Nanjing, Xiamen, Guangzhou, Chengdu, Shenyang, Qingdao, Ningbo, Xian, Haerbin, Jinan, Changchun na Lasha. Licha ya hayo China imechagua miji 10 ikiwemo ya Haerbin, Jilin, Zhengzhou, Zahoqing, Liuzhou na Qingdao, kuwa miji maarufu ya kiutamaduni.

BEIJING

     Beijing ni mji mkuu wa China, na ni kitovu cha siasa na utamaduni nchini China. Beijing iko katika sehemu ya kaskazini ya ardhi ya tambarare ya kaskazini ya China. Kijiografia, Beijing, Rome ya Italia, Madrid ya Hispania ziko katika latitudo moja. Hali ya hewa ya Beijing ni yenye upepo wa kimajira wa bara, siku za majira ya baridi na joto ni nyingi, siku za majira ya kichipuka na kupukutika ni kidogo na kukosa mvua. Wastani wa hali-joto ni nyuzi 11.8 sentigredi kwa mwaka.
Beijing ina historia ndefu sana ya kuanzia miaka 3,000 iliyopita. Katika kipindi cha mwaka 770 hadi mwaka 221 K.K, sehemu ya Beijing ilikuwa mji mkuu wa nchi ndogo za himaya ya ufalme, katika enzi za Qin na Han pamoja na kipindi cha Nchi Tatu, Beijing ilikuwa mmoja wa mji muhimu katika sehemu ya kaskazini ya China. Beijing ilianza kuwa mji mkuu wa nchi tangu enzi ya Jin, ikifuatiwa na enzi za Yuan, Ming na Qing, ambapo kulikuwa na wafalme 34 waliotawala dola kutokea Beijing.
Baada ya kuasisiwa China mpya, hususan katika miaka zaidi 20 iliyopita baada ya kuanza kutekeleza sera za mageuzi na ufunguaji mlango, sura ya Beijing ilikuwa na mabadiliko makubwa. Majengo ya kisasa yalijengwa kila mahali na uhusiano na nchi za nje ulikuzwa kwa mfululizo. Hivi sasa, Beijing, inapiga hatua kubwa kuingia kwenye kundi la miji mikubwa duniani. Beijing, ambayo mabaki ya historia yameungana vizuri na sura ya kisasa, inavutia watu wa sehemu mbalimbali. Katika miaka ya karibuni, Beijing kila mwaka imekuwa inapokea mamilioni ya watalii kutoka nchi za nje na milioni ya makumi ya watalii wa nchini.
Historia ndefu iliiachia Beijing vitu vingi vya kale pamoja na utamaduni murua wa jadi. Ikiwa unapenda vitu na mabaki ya utamaduni, unaweza kwenda kuona Ukuta Mkuu, kutembelea makasri makubwa, au kutembelea bustani za kifalme ambazo ni pamoja na Summer Palace, Beihai, Xiangshan na Tiantan. Mandhari nzuri na majengo makubwa ya huko yatafanya wewe kutoka kuondoka. Ikiwa unataka kufahamu utamaduni na mambo kuhusu watu mashuhuri wa China, unaweza kutembelea maskani mengi ya watu mashuhuri au kwenda kusikiliza Beijing opera. Ikiwa unataka kujua hali ya maendeleo ya maeneo mbalimbali ya siasa, uchumi, sayansi na teknolojia na kijeshi, unaweza kwenda kutembelea majumba ya makumbusho zaidi ya mia moja yaliyoko mjini Beijing. Ukitaka kujiburudisha kwa mandhari nzuri ya kimaumbile ya Beijing, unaweza kwenda kuangalia milima na mito iliyoko katika sehemu ya mzunguko wa Beijing.
Hivi sasa, sehemu za mandhari ya ngazi ya 4A zilizoko hapa Beijing ni pamoja na Tiantan, makaburi 13 ya enzi ya Ming, Summer Palace, Jumba la wanyama wa baharini la Beijing, Ukuta Mkuu wa Badaling, Mlima wa Jing, Bustan ya Beihai, bustani ya makabila ya China, Jumba la sayansi na teknolojia la China, bustani ya wanyama la Beijing na Bustani ya mimea ya Beijing.


XIAN

       Xian, ambayo iko katika sehemu ya kaskazini magharibi ya China, ni mji mkuu wa mkoa wa Shanxi na kuchukuliwa kuwa ni kitovu cha siasa, uchumi na mawasiliano cha sehemu ya kaskazini magharibi na China bara.
Mji wa Xian ni mmoja kati ya miji sita ya kale ya China ambayo ni Xian, Luoyang, Nanjing, Kaifeng, Hangzhou na Beijing. Xian ni mji mkuu wa enzi nyingi na kwa muda mrefu zaidi kuliko miji mingine ya kale, na kujulikana sana kwa historia na utamaduni wake. Katika historia ya China, wataalam wa elimu ya historia wamethibitisha kuwa enzi 10 za Zhou ya magharibi, Qin, Han ya magharibi, Zhao ya awali, Qin ya baadaye, Wei ya magharibi, Zhou ya kaskazini, Sui na Tang zilichagua Xian kuwa ni mji mkuu. Hivyo, mji wa Xian wenye historia ya zaidi ya miaka elfu moja, una athari kubwa katika historia na ni wa kipekee ukilinganishwa na miji mingine.
Xian, ambao unachukuliwa kuwa ni mmoja kati ya miji minne ya kale duniani, ni sehemu maarufu ya utalii. Sanamu za askari na farasi wa mfalme Qingshihuang, ambazo zinasifiwa kuwa ni “ajabu kubwa la nane duniani” ziko katika wilaya ya Lintong ya mji wa Xian, sanamu za askari na farasi ni zaidi ya 6,000 kwa jumla, na kuchukuliwa kuwa ni ugunduzi mkubwa kabisa wa karne ya 20. Licha ya hayo kuna sehemu nyingine za mandhari nzuri zikiwa ni pamoja na Mnara wa Wide Goose, Dimbwi la Huaqing, na mlima wa Hua. Picha hiyo ni Ukumbi wa makumbusho ya sanamu za askari na farasi za mfalme Qinshihuang.

LAHSA

     Lahsa ni mji mkuu wa mkoa unaojiendesha wa Tibet, China, ambao uko katika upande wa kaskazini wa mlima wa Himalaya, eneo lake ni kilomita za mraba 29,052. hali ya hewa ya Lahsa ni ya uwanda wa juu, kuna siku nyingi zenye jua, mvua kidogo, hakuna baridi kali katika majira ya baridi wala joto kali katika majira ya joto, wastani halijoto katika mwaka ni sentigredi nyuzi 7.4; Mvua hunyesha katika miezi mitatu ya 7, 8 na 9, na kiwango cha mvua ni kiasi cha milimita 500; Jua linawaka kwa saa zaidi ya 3,000 kwa mwaka, hivyo Lahsa unajulikana kuwa ni “mji wa mwangaza”. Lahsa ina hewa safi, jua nzuri, mchana ni joto kiasi na usiku ni baridi, hivyo ni sehemu nzuri sana ya kukwepa joto kali katika majira ya joto.
Lahsa iko katika uwanda wa juu wa Qinghai na Tibet, ambao unajulikana kama “paa la dunia”, uko katika wastani wa mita 3,600 juu ya usawa wa bahari, hakuna hewa ya oxygen ya kutosha, ina upungufu wa hewa hiyo kwa kati ya 25% hadi 30% ikilinganishwa na sehemu nyingine za China bara. Katika siku za mwanzoni watu husikia maumivu ya kichwa na kupumua kwa haraka. Katika siku ya kwanza baada ya kufika Lahsa, mtu anapaswa kupumzika ili kuzoea hali ya huko. Kipindi cha kati ya mwezi Aprili na Oktoba ni kizuri kwa utalii huko Tibet. Katika lugha ya Kitibet, Lahsa ni mahali patakatifu anapokaa mungu. Mji wa Lahsa umekuwa na historia ndefu na jadi ya kidini, sehemu za utalii mjini ni pamoja na hekalu ya Dazhao, mtaa wa Baguo na kasri la Budala.
(picha hiyo ni kasri la Budala ya Lahsa)