KIVUTIO CHA MIJI MIDOGO YA CHINA

中国国际广播电台

      
Miji ya China ina historia ndefu, hususan baadhi ya miji midogo iliyojengwa zaidi ya miaka mia moja iliyopita, inavutia watu zaidi, kwa mfano, mto Li wa mkoa wa Yunnan umeorodheshwa kuwa ni urithi wa utamaduni duniani. Historia na utamaduni wa miji midogo pamoja na siku za jana na leo zimeanza kutembelewa na watalii wa nchini na wa nchi za nje.


TARAFA YA ZHOUZHUANG

      Tarafa ya Zhouzhuang iko katika mkoa wa Jiangsu, sehemu ya mashariki ya China, umbali wa kilomita 38 tu kutoka mji wa kale wa Suzhou. Mchoraji mashuhuri wa michoro ya kichina Bw. Wu Guanzhong aliwahi kuandika makala ikisema kuwa Mlima Manjano umekusanya uzuri wa milima ya China, na tarafa ya Zhouzhuang imekusanya uzuri wa vijiji vyenye mito na maziwa”, magazeti ya nchi za nje yanasifu Zhouzhuang kuwa ni “tarafa ya kwanza yenye mito na maziwa nchini China”.
Tarafa ya Zhouzhuang inazungukwa na maziwa ya Deng, Baiyan, Dingshan, na Nan pamoja na mito ya wastani na midogo zaidi ya 30, nyumba za wakazi zote zimejengwa kando ya mito, ambazo ni nyumba za mtindo wa kale na zenye ua. Zaidi ya 60% nyumba za tarafa hiyo zilijengwa katika enzi za Ming na Qing, tarafa hiyo ya kale yenye kilomita ya mraba 0.4, ina nyumba za mtindo wa kale karibu 100, pamoja na malango makubwa zaidi ya 60 yaliyojengwa kwa matofali. Licha ya hayo, tarafa ya Zhouzhuang imehifadhi vizuri madaraja 14 yenye utaalamu wa kale, mandhari ambayo ni kama watu wanavyosema kuwa “madaraja madogo, mito na nyumba za wakazi”. Mazingira ya Zhouzhuang ni mazuri na hayana makelele, hivyo ni sehemu nzuri za kusoma, wenyeji wa huko wana jadi ya kusoma, katika historia walijitokeza wasomi wakubwa zaidi ya 20. Wasomi na washairi wengi kutoka sehemu nyingine walitunga mashairi na kuchora michoro juu ya uzuri wa tarafa hiyo. Mfasihi wa enzi ya Jin ya magharibi Zahng Han, washairi wa enzi ya Tang Li Yuxi na Lu Guimeng waliwahi kukaa katika tarafa ya Zhou.

      Mandhari muhimu ya tarafa ya Zhou ni pamoja na hekalu la Quanfu, chuo cha dini ya Dao cha Chengxu, Ukumbi wa Shen, daraja la Fuan na Jumba la mi. Tarafa ya Zhou iko katikati ya Suzhou na Shanghai, mawasiliano ni mepesi sana, kuna mabasi yanayofika huko moja kwa moja. Kwa kuwa Zhouzhuang iko karibu na Shanghai, hivyo, watalii wanaweza kwenda na kurudi kwa siku moja, huko hakuna mahoteli mengi ya ngazi ya nyota, lakini nyumba za kawaida za wageni ni nyingi, ingawa nyumba hizo siyo za hali ya juu, lakini ni safi sana.


MJI WA KALE WA PHOEINIX

       Tarafa ya Phoenix iko katika wilaya inayojiendesha ya makabila ya watuju na wamiao, sehemu ya magharibi ya mkoa wa Hunan, katikati ya China.“Mji wa kale wa Phoeinix” unaoitwa na mwandishi wa vitabu wa New Zealand Luis Ari kuwa ni mmoja wa mji mdogo nzuri kabisa nchini China, ulijengwa katika nasaba ya Kangxi ya enzi ya Qing. Mji huo unaojulikana kwa “Lulu ya magharibi ya mkoa wa Hunan” ni mdogo kweli kweli, na kuna barabara moja tu mjini humo.


Mji wa kale wa Phoenix una sehemu mbili za mji wa kale na mji mpya, mji wa kale uko kando ya mto, chini ya mlima, mto Tuo unapita katikati ya mji, ukuta mrefu wa mji ulijengwa kwa mawe mekundu kando ya mto, na mlima wa Nanhua uko karibu na mji wa kale. Ngome ya mji ulijengwa katika enzi ya Qing. Katika mto mpana ulioko karibu sana na mlango mkubwa wa kaskazini wa mji, lilijengwa daraja moja jembamba, watu wawili wakikutana kwenye daraja hilo, hawana budi kugeuza miili yao ili mmoja kumpisha mwenzie. Daraja hilo lilikuwa daraja pekee la kutokea nje kwa wakazi wa mji huo.
Tarafa ya Phoenix imejulikana kutokana na kuwa ni maskani ya mwanzo kabisa ya mwandishi vitabu mashuhuri Shen Congwen wa miaka ya karibuni. Maskani ya mwandishi vitabu huyo alikaa ndani sana ya kichochoro kimoja kilichotandikwa vipande vya mawe kwenye mtaa wa Ying wa mji huo wa kale. Nyumba yake ilijengwa kwa matofali na mbao ni kama nyumba ya kijadi ya Beijing. Sehemu muhimu ya mandhari ya tarafa ya Phoenix ni pamoja na kuangalia jua likichomoza katika mlima wa mashariki, misitu ya mlima wa Nanhua, makengele yakilia katika hekalu iliyojengwa mlimani, mashua za wavuvi zenye kandili katika usiku na kuangalia mbalamwezi kwenye daraja na Xi. Watalii wanaweza kuwasili mji wa Jishou mkoani Hunan kwa ndege kisha kutumia mabasi.