|
|
|
|
|
HALI YA VITOWEO VYA CHINA
|
|
中国国际广播电台
Vitoweo vya China vimegawanyika
katika aina nane kutokana na
umaalumu wa mapishi yake, zikiwa
ni pamoja na Shandong, Sichuan,
Guangdong, Fujian, Jiangsu,
Zhejiang, Hunan na Anhui.
Kukamilika kwa aina moja ya
vitoweo kunahitaji miaka mingi
na umaalumu wa mapishi yake,
vilevile kunaathiriwa na hali
za kijiografia, hewa, rasilimali
na mazoea ya chakula. Kulikuwa
na mtu aliyefananisha mapishi
ya vitoweo ya Jiangsu na Zhejiang
kama warembo wembamba wa sehemu
ya kusini ya China; Vitoweo
vya mikoa ya Shandong na Anhui
kama watu makamo wenye nguvu
wa sehemu ya kaskazini; vitoweo
vya mikoa ya Guangdong na Fujian
kama vijana watanashati; Na
vitoweo vya mikoa ya Sichuan
na Hunan kama wasomi wenye ujuzi
na elimu nyingi.
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|