|
|
|
|
|
Mambo kuhusu visa ya utalii nchini China |
|
中国国际广播电台
Ikiwa ni hatua ya kwanza kwa
wewe kutembelea China, unapaswa
kuishughulikia visa ya utalii.
Wageni wanapaswa kuomba visa
kwenye ofisi ya ubalozi ya China
katika nchi za nje. Watalii
zaidi ya 9 wakitaka kuitembelea
China wanaweza kuomba visa ya
utalii ya kikundi. Kwa wageni
wanaotembelea mikoa maalumu
ya kiuchumi ya Shenzhen, Zhuhai
na Xiamen wanaweza kuomba visa
ya utalii moja kwa moja kwa
ofisi za forodha za mikoa hiyo.
Wageni wale wanaotembelea mkoa
wa Hainan kwa muda usiozidi
siku 15, wanaweza kuomba visa
kwenye ofisi za forodha za miji
ya Haikou na Sanya. Wageni wanaotembelea
Shenzhen kwa muda usiozidi saa
72 kutoka Hong Kong, hawana
haja ya kuomba visa. Wageni
waliopata visa wanatakiwa kuingia
China kupitia forodha zilizofunguliwa
kwa wageni au forodha walizoelezwa
baada ya kushughulikiwa na wafanyakazi
wa forodha.
Watalii wa kigeni wenye pasipoti
na visa ya utalii wanaweza kufanya
matembezi katika sehemu zilizosofungua
mlango kwa nchi za nje, serikali
ya China inalinda maslahi halali
za wageni walioko nchini, lakini
hawaruhusiwi kufanya shughuli
zisizolingana na hali yao, zikiwa
ni pamoja na ajira, kueneza
dini na kufanya mahojiano na
watu bila kibali, la sivyo watachukuliwa
hatua. Aidha, wanapokuwa nchini
China wanapaswa kuheshimu sheria
na mila za China.
Watalii wanaweza kufanya matembezi
nchini China katika muda waliopewa.
Endapo wanataka kuendelea kufanya
matembezi baada ya kupita muda
wao, wanaweza kuziomba idara
za usalama za karibu kurefusha
muda wa matembezi. Baada ya
kumaliza matembezi wanatakiwa
kuondoka China kupitia forodha
za kimataifa zilizofunguliwa
kwa wageni.
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|