Mambo unayopaswa kujua wakati unapopita kwenye forodha ya China
中国国际广播电台

  Mgeni anapopita kwenye forodha ya China anatakiwa kufuata maagizo husika ya forodha ya China, ili kufanikisha matembezi yako na kupita kwenye forodha bila matatizo, anatakiwa kufahamu mambo yafuatayo:
Mtalii anaondoka China akichukua au kusafirisha vitu vinavyo orodheshwa hapo chini, anatakiwa kuieleza forodha:

Vitu vinavyotozwa ushuru, na kiasi cha vitu vinavyoingia nchini bila kulipa ushuru
Vitu vinavyotumiwa na wasafiri wenyewe safarini pamoja na vitu ambavyo haviko katika eneo la vitu vinavyotumiwa na wasafiri wenyewe safarini, lakini bado vinahesabiwa kuwa ni vitu wanavyohitaji safarini;
Vitu vinavyopigwa marufuku kuingia au kutoka China pamoja na kiasi cha vitu vinavyoruhusiwa kuingia na kutoka China vikiwa ni pamoja na vitu vya kale, sarafu, dhahabu, fedha pamoja na vitu vilivyotengenezwa kwa madini hayo, maandishi yaliyochapishwa, na kaseti za audio na video;
Bidhaa, sampuli za bidhaa na vitu ambavyo haviko katika eneo la mizigo ya watalii.

NJIA ZA RANGI NYEKUNDU NA KIJANI

Wasafiri wanaotakiwa kulipa ushuru na wale waliohitaji kibali kwa mizigo yao wapite kwenye “njia nyekundu”; wasafiri wengine wanaweza kupita kwenye “njia ya rangi ya kijani”.

KANUNI ZA KAWAIDA

Kwa kawaida, msafiri anapopita kwenye forodha, mizigo yote aliyokuwa nayo inatakiwa kukaguliwa. Mizigo ambayo haijakubaliwa na forodha haichukuliwi au kusafirishwa.
Mizigo yake iliyosafirishwa, ambayo haikuwa pamoja na msafiri inatakiwa kutolewa maelezo katika “fomu ya mizigo ya msafiri”, na inatakiwa kuingia au kutoka nchini katika muda wa miezi 6 baada ya msafiri kuingia au kutoka China.
“Fomu ya mizigo ya msafiri” iliyosainiwa na mfanyakazi wa forodha inatakiwa kutunzwa vizuri ili ashughulikiwe haraka wakati atakapoondoka au kuingia nchini.
Aidha, msafiri anapaswa kutoa maelezo kwa forodha wakati anapoondoka China akichukua vitu vya mabaki ya kiutamaduni. Vitu vya mabaki ya kiutamaduni alivyonunua msafiri katika maduka yenye leseni ya biashara ya mabaki ya kiutamaduni, forodha inamruhusu kuondoka baada ya kukagua risiti maalumu za biashara hiyo yenye muhuri wa idara ya usimamizi wa mabaki ya kiutamaduni ya China. Msafiri akitaka kuondoka nchini na kuchukua vitu vya mabaki ya kiutamaduni ambavyo alivipata kwa njia nyingine vikiwa ni pamoja na kurithi kutoka wazazi au kupewa zawadi na marafiki, anapaswa kuthibitishwa na idara ya usimamizi wa vitu vya mabaki ya kiutamaduni ya China. Hivi sasa, idara hiyo imefungua ofisi zake katika forodha za miji minane ikiwemo ya Beijing, Shanghai, Tianjin na Guangzhou. Vitu vinavyoruhusiwa kuchukuliwa katika nchi za nje baada ya kuthibitishwa na kupewa kibali na idara ya usimamizi wa mabaki ya vitu vya kiutamaduni vinakubaliwa kupita kwenye forodha ya China.