MAELEZO KUHUSU KARANTINI
中国国际广播电台

      Idara ya karantini ya China ni idara ya utekelezaji wa sheria iliyoanzishwa kutokana na agizo la serikali kuhusu shughuli za karantini zinaohusika na nchi za nje, idara hiyo na vitengo vilivyo chini yake katika forodha zilizofunguliwa mlango kwa nchi za nje kufanya ukaguzi wa karantini kwa mujibu wa sheria juu ya watu wanaoingia na kutoka nchini, na forodha zinatoa ruhusa ya kuingia au baada ya kuona vyeti vilivyosainiwa na vitengo vya karantini.
Vyombo vya mawasiliano, watu, chakula, maji ya kunywa pamoja na wadudu na maradhi ya kuambukiza vinafuatiliwa zaidi.
Vitengo vya karantini vinawazuia wageni wenye baadhi ya magonjwa kuingia nchini, ambao ni pamoja na wenye virusi vya ukimwi, magonjwa ya zinaa ya kuambukiza na kifua kikuu kilichoko katika kipindi cha kuambukiza.