Kuandaa na Kuteua Makada wa makabila Madogo

Radio China Kimataifa

Serikali ya China inatilia maanani sana kazi ya kuandaa makada wa makabila madogo. Idadi ya makada wa makabila madogo imeongezeka kwa kiwango kikubwa, na wameshika nyadhifa za uongozi katika ngazi tofauti. Hivi sasa nyadhifa za wenyekiti wa mikoa mitano inayojiendesha, na wakuu wa tarafa 30 na wilaya 119 zinazojiendesha ni zinachukuliwa na makada wa makabila madogo.

Watu wa makabila mbalimbali wanashiriki katika usimamizi wa mambo ya kisiasa na kijamii. Katika bunge la umma na baraza la halmashauri ya kisiasa ya China, makabila 56 yana wajumbe au wawakilishi wake, ambao wanachukua zaidi ya asilimia 10.