Majengo ya Bustani

中国国际广播电台

      

Majengo ya bustani nchini China yana historia ndefu, na ni majengo maarufu duniani. Mapema miaka 3000 iliyopita kulikuwa na bustani ya kifalme nchini China. Tokea hapo bustani zilianza kuwepo katika miji mikuu ya enzi mbalimbali na miji mingine mikubwa. Kuna aina nyingi za bustani nchini China ambazo ni muhimu katika mifumo mitatu mikuu ya ujenzi wa bustani duniani.

Bustani nchini China huwa na milima na maji kwa ajili ya kuleta uzuri wa kimaumbile.

Majengo ya bustani nchini China yanagawanyika katika fungu la bustani za kifalme na bustani binafsi. Bustani hizo zilijengwa kwa milima ya bandia na maziwa, maua na miti, nyua za nyumba, na ujia wenye paa na mbao zenye maandishi, bustani yenye mzingira hayo ni kama bustani ya peponi. Bustani nchini China zimegawanyika kwa dhana za aina tatu, yaani dhana za utawala wa kifalme, dhana za mandhari ya kichimbakazi (fairyland) na dhana za mandhari ya kufananisha na hali ya maumbile.

Mandhari ya kichimbakazi yanazingatia kuleta mazingira ya utawa, mazingira ambayo yalifuatwa sana na waumini wa dini ya Dao ya Kichina. Mazingira kama hayo pia yanaonekana katika ujenzi wa mahekalu na bustani za kifalme.

Mandhari ya kufananisha na maumbile yanajengwa kwa kufuata hisia za wenye bustani. Mandhari za namna hiyo zinapatikana zaidi katika bustani za wasomi.
Tofauti kubwa kati ya bustani za Kichina na za Kimagharibi ni kuwa bustani za Kimagharibi zinajengwa kwa kuonesha uzuri wa majengo, na bustani za Kichina zinajengwa kwa nia ya kuonesha uzuri wa mandhari ya kimaumbile na hisia za wenye bustani.

 

Bustani katika Mji wa Suzhou
Bustani kadhaa mjini Suzhou ziliorodheshwa katika kumbukumbu ya urithi wa dunia mwaka 1997. Bustani katika mji huo zimeingiza sifa zote za bustani nchini China. Bustani hizo zimekuwa na miaka zaidi ya 2000, na zilizobaki sasa ziko 10. Bustani katika mji wa Suzhou nyingi ni ndogo, lakini kutokana na kuwa ndani yake kuna milima ya bandia na maziwa, miti na maua, madaraja madogo na vibanda, bustani hizo zinaonekana mandhari kubwa ya kimaumbile na kufanya watu wahisi wako kwenye mazingira ya utamaduni mkubwa.


Bustani ya Kifalme Yuanmingyuan
Bustani hiyo ya kifalme ilikuwa na mchanganyiko wa mitindo ya Kichina na Kimagharibi. Hii ilikuwa ni bustani nzuri kuliko zote nchini China. Lakini mwaka 1860 bustani hiyo iliteketezwa na muungano wa wavamizi wa Uingereza na Ufaransa. Hivi sasa watu wanaweza tu kukisia jinsi ilivyokuwa nzuri kwa kuangali magofu yake.

Bustani ya Kifalme ya Yuanmingyuan iko katika kitongoji cha Beijing upande wa kaskazini magharibi. Bustani hiyo licha ya kuwa bustani nzuri kuliko bustani nyingine za kifalme pia imewahi kujulikana hata barani Ulaya kutokana na maelezo ya barua za wamisionari na ilikuwa na athari kwa ujenzi wa bustani za Ulaya.