中国国际广播电台
Ujenzi wa makaburi ni sehemu
muhimu katika ujenzi wa China
ya kale. Kutokana na imani
ya wahenga wa China kuwa roho
ya marehemu inadumu milele,
mazishi yalikuwa yakitiliwa
maanani sana, kwa hiyo watu
walikuwa makini sana katika
ujenzi wa makaburi. Katika
historia ndefu nchini China
ujenzi wa makaburi ulipata
maendeleo makubwa na makaburi
mengi maarufu ya wafalme na
malkia yalijengwa. Kutokana
na jinsi muda ulivyokuwa ukipita,
ujenzi wa makaburi ulichanganywa
na sanaa za uchoraji na uchongaji
wa sanamu, na kuyafanya makaburi
yawe na mkusanyiko wa sanaa
za aina nyingi.
Ujenzi wa makaburi nchini
China ni mkubwa na wenye majengo
mengi. Kwa kawaida ujenzi
huo hutumia vizuri sura ya
kimaumbile ya ardhi kwenye
milima, ingawa pia kulikuwa
na makaburi yaliyojengwa katika
sehemu za tambarare. Kwa kawaida
mpangilio wa majengo ya makaburi
huwa na uzio unaozunguka sehemu
ya kaburi, na kila upande
kuna mlango mmoja, na kwenye
kila kona ya uzio kuna jumba
la ghorofa, mbele ya kaburi
kuna barabara na kwenye pande
mbili za barabara kuna sanamu
kubwa za mawe za wanyamapori
na askari walinzi, ndani ya
uzio huo imepandwa misonobari
mingi, mazingira hayo yaliwafanya
watu kuwa na heshima kubwa
kwa marehemu katika hali ya
ukimya kabisa.
Kaburi la Mfalme Qinshihuang
Kaburi la mfalme Qinshihuang
(259K.K.-210K.K.) liko nje ya
mji wa Xi’an mkoani Shanxi upande
wa kaskazini mwa Mlima Lishan,
hilo ni moja ya makaburi maarufu
nchini China. Kaburi hilo lilijengwa
miaka 2000 iliyopita. Sanamu
za askari na farasi zinazosifiwa
kuwa ni moja ya “maajabu nane
duniani” ni “walinzi wa kaburi”
hilo. Sanamu hizo ziliwekwa
na UNESCO katika orodha ya urithi
wa dunia mwaka 1987. Kamati
ya Urithi wa Dunia ilisema,
“Sanamu zenye sura mbalimbali
za askari, farasi na mikokoteni
ya kivita iliyoko pembezoni
mwa kaburi la mfalme Qinshihuang
ni sanaa adimu aidha iwe katika
zama hizi au za kale, zina thamani
kubwa za kihistoria.
Sehemu iliyo
karibu na mji wa Xi’an lina
makaburi mengi ya wafalme,
licha ya kaburi la mfalme
Qinshihuang, kuna makaburi
11 ya wafalme wa Enzi ya Han
Magharibi (206 K.K.-220) na
18 ya wafalme wa Enzi ya Tang
(618-907).
Makaburi ya Wafalme
wa Enzi ya Ming na Qing
Makaburi ya wafalme wa Enzi
ya Ming na Qing ni makaburi
ya wafalme yaliyohifadhiwa
kikamilifu nchini China.
Makaburi hayo yako katika
kitongoji cha Changping nje
ya Beijing chini ya mlima
Tianshoushan, wafalme 13 walizikwa
huko baada ya mji mkuu wa
Enzi ya Ming kuhamishwa kwenye
mji wa Beijing kutoka mji
wa Nanjing. Makaburi hayo
yako katika bonde lililozungukwa
na milima kwa pande tatu.
Kwenye mteremko wa mlima yalipangwa
makaburi hayo 13, eneo la
makaburi ni kilomita 40 za
mraba. Katika sehemu hiyo
wamezikwa wafalme 13, malkia
23 na wake wenzao, watoto
na mabinti wa wafalme.
Makaburi ya wafalme 13 wa
Enzi ya Ming yalijengwa kwa
adhama kubwa na penye mandhari
nzuri, ni fungu kamili la
makaburi ya wafalme nchini
China. Kati ya makaburi hayo,
kaburi la Changling yaani
kaburi la mfalme wa tatu,
Zhuli, na kaburi la Ding yaani
kaburi la mfalme wa 14 wa
enzi ya Ming, Zhuyi, ni makaburi
makubwa zaidi. Baada ya kufukuliwa,
watu wamegundua kuwa ukumbi
wa ardhini bado ni madhubuti
ambao ulijengwa kwa mawe wenye
nusu duara ya paa kwa mawe,
pembeni mwa ukumbi huo kuna
mitaro ya maji, na tao la
mawe halikutitia, ikionesha
ufundi mkubwa wa ujenzi wa
ukumbi huo katika China ya
kale.
Sehemu ya mashariki nje ya
Beijing kuna eneo la kilomita
za mraba 78 za makaburi ya
wafalme wa Enzi ya Qing (1616-1991),
sehemu ya makaburi ni kilomita
za mraba 78, wafalme watano
na malkia 14 wa Enzi ya Qing
walizikwa huko. Huko makaburi
yote yalijengwa kwa makini
na ufahari.
|