Majengo katika Enzi ya Tang

中国国际广播电台

       Enzi ya Tang (618-907) ni kipindi ambacho uchumi na utamaduni katika jamii ya kimwinyi nchini China ulifikia kwenye kilele, ufundi na sanaa za ujenzi wa majengo pia zilikuwa zimeendelea sana. Majengo katika Enzi ya Tang yalikuwa makubwa na ya adhama.

Majengo katika Enzi ya Tang yalikuwa ni makubwa, na mpangilio wa fungu la majengo ni wa busara. Katika mji mkuu wa Enzi ya Tang, Chang An (mji wa Xi’an kwa leo), na mji wa Luoyang kuna makasri makubwa na majumba ya maofisa. Mji wa Chang An ulikuwa mji mkubwa duniani katika enzi hiyo, na mpangilio wa majengo yake ulikuwa wa busara kabisa katika miji yote ya China ya kale, ndani ya mji huo kasri la Daming lilikuwa na eneo zaidi ya mara tatu kuliko Kasri la Kifalme la Beijing.

Majengo katika Enzi ya Tang yanaonesha sayansi ya muundo wa mbao, mshikamano baina ya nguzo na maboriti umeonesha ushirikiano mzuri wa nguvu. Ukumbi wa Buddha katika Hekalu la Foguang mlimani Wutaishan umeonesha wazi mtindo wa majengo ya Enzi ya Tang.
Kadhalika, majengo ya matofali na mawe pia yalikuwa yameendelea sana katika Enzi ya Tang, mifano ya majango hayo ni pagoda ya Dayanta, pagoda ya Xiaoyanta na pagoda ya Qianxunta katika mji wa Xi’an.