中国国际广播电台
Enzi ya Song (960-1279) ilikuwa
ni enzi iliyodidimia katika
siasa na mambo ya kijeshi, lakini
uchumi, viwanda vya kazi za
mikono na biashara vilikuwa
na maendeleo kwa kiasi fulani,
na hasa katika sayansi na teknolojia,
hali hiyo iliufanya ufundi wa
majengo ufikie kiwango kipya.
Majengo katika enzi hiyo yalibadilika
kuwa madogo na yenye makini
ya mapambo badala ya yale ya
majengo makubwa na ya adhama
ya Enzi ya Tang.
Katika miji ya Enzi ya Song
yalitokea maduka kwenye barabara,
na maduka yalipangwa kwa aina
ya bidhaa, na majengo ya shughuli
za zimamoto, mawasiliano,
uchukuzi, maduka na madaraja,
yote yaliendelea kwa hatua
kubwa. Sura ya mji mkuu wa
Enzi ya Song, Bianliang, (mji
wa Kaifeng kwa leo) ilionesha
wazi hali ya biashara katika
miji ya Enzi ya Song. Katika
enzi hiyo, nchini China majengo
makubwa makubwa hayakujengwa
sana, lakini mapambo na rangi
za majengo yalizingatiwa zaidi.
Ukumbi katika hekalu la Jinxi
mkoani Shanxi ni mfano wa
majengo hayo.
Majengo ya matofali yaliendelea
zaidi katika Enzi ya Song,
majengo hayo yalikuwa ni pagoda
ya dini ya Buddha na madaraja.
Pagoda katika hekalu la Huilingsi
mkoani Zhejiang, pagoda la
Fanta katika mji wa Kaifeng
mkoani Henan na daraja la
Yongtong wilayani Zhaoxian
mkoani Hebei yote yanastahili
kuwa kama ni mifano ya majengo
ya matofali katika Enzi ya
Song.
Uchumi wa Enzi ya Song uliendelea
kwa kiasi fulani, katika enzi
hiyo, ujenzi wa bustani ulianza
kustawi. Ujenzi wa bustani
ulitilia mkazo muunganisho
wa uzuri wa bandia na wa kimaumbile,
bustani katika enzi hiyo ilikuwa
inapambwa kwa milima bandia,
maji, maua na miti ili kuleta
mazingira kama ya kimaumbile.
Katika Enzi ya Song kulikuwa
na kitabu cha “Ufundi wa Ujenzi
wa Nyumba”. Kitabu hiki kinaeleza
kanuni za usanifu na ufundi
wa ujenzi wa nyumba, ambacho
kinaonesha kuwa ujenzi wa
nyumba katika Enzi ya Song
ulikuwa umefikia kiwango kipya.
|