Majengo ya Enzi ya Yuan

中国国际广播电台

       Enzi ya Yuan (1206-1368) nchini China ilikuwa ni dola la kifalme lililoundwa na watawala wa kabila la Wamongolia, lakini katika enzi hiyo, majengo hayakuwa na maendeleo, na majengo mengi yalikuwa ya kawaida kutokana na kuzorota kwa uchumi na utamaduni.

Mji mkuu wa Enzi ya Yuan, Dadu (sehemu ya kaskazini ya Beijing kwa leo) ni mwanzo wa mji mkuu wa enzi mbili za Ming na Qing, Beijing. Shughuli za ujenzi katika mji mkuu huo zilikuwa hasa katika ujenzi wa majengo ya ukumbi na bustani, Bustani ya Beihai ya leo mjini Beijing ni kumbukumbu halisi ya enzi hiyo.

Katika Enzi ya Yuan dini ilikithiri sana, hasa dini ya Buddha ya madhehebu ya Kitibet, kwa hiyo mahekalu ya dini yalikuwa mengi.

Majengo ya mbao katika Enzi ya Yuan yaliurithi ufundi wa enzi iliyotangulia ya Song, lakini kutokana na uchumi uliokuwa mbaya na uhaba wa magogo, majengo katika enzi hiyo yalikuwa ya kawaida yakilinganishwa na majengo ya Enzi ya Song iwe kwa ukubwa au kwa umakini.