中国国际广播电台
Kuanzia Enzi ya Ming (1368-1644)
China iliingia katika kipindi
cha mwisho cha jamii ya kimwinyi.
Mitindo ya majengo katika enzi
hiyo mingi zaidi ilirithi mitindo
ya majengo ya enzi iliyotangulia
ya Song bila kuwa na mabadiliko
makubwa, lakini ukubwa wa majengo
uliongezeka kwa ajili ya kuonesha
adhama.
Katika enzi hiyo, mpangilio
wa ujenzi wa mji na majengo
ya makasri yote yalirithishwa
na watu wa baadaye. Majengo
yaliyobaki sasa katika mji
wa Beijing na Nanjing yote
yalianzia enzi hiyo ya Ming,
na enzi iliyofuata ya Qing
ilipanua na kuimarika tu katika
msingi wa enzi ya Ming. Mji
wa Beijing wa enzi ya Qing
ulijengwa kwa msingi wa mji
wa enzi ya Ming, mji huo unagawanyika
mji wa ndani, wa nje na mji
wa kifalme.
ukuta
mkuu
Katika enzi ya Ming, jengo
kabambe la kujikinga dhidi
ya maaduni yaani Ukuta Mkuu
liliendelea kujengwa, na ufundi
wa jengo hilo ulikuwa ni wa
hali ya juu kuliko zamani.
Ukuta huo katika enzi ya Ming
ulianzia ukingo wa Mto Yalujiang
kutoka mashariki na kufikia
Jiayuguan upande wa magharibi,
jumla una urefu wa kilomita
5660, na kipande cha ukuta
huo cha Badaling kiungani
mwa Beijing kina thamani kubwa
katika sanaa.
|