Majengo ya Enzi ya Ming

中国国际广播电台

       Kuanzia Enzi ya Ming (1368-1644) China iliingia katika kipindi cha mwisho cha jamii ya kimwinyi. Mitindo ya majengo katika enzi hiyo mingi zaidi ilirithi mitindo ya majengo ya enzi iliyotangulia ya Song bila kuwa na mabadiliko makubwa, lakini ukubwa wa majengo uliongezeka kwa ajili ya kuonesha adhama.

Katika enzi hiyo, mpangilio wa ujenzi wa mji na majengo ya makasri yote yalirithishwa na watu wa baadaye. Majengo yaliyobaki sasa katika mji wa Beijing na Nanjing yote yalianzia enzi hiyo ya Ming, na enzi iliyofuata ya Qing ilipanua na kuimarika tu katika msingi wa enzi ya Ming. Mji wa Beijing wa enzi ya Qing ulijengwa kwa msingi wa mji wa enzi ya Ming, mji huo unagawanyika mji wa ndani, wa nje na mji wa kifalme.

ukuta mkuu

       Katika enzi ya Ming, jengo kabambe la kujikinga dhidi ya maaduni yaani Ukuta Mkuu liliendelea kujengwa, na ufundi wa jengo hilo ulikuwa ni wa hali ya juu kuliko zamani. Ukuta huo katika enzi ya Ming ulianzia ukingo wa Mto Yalujiang kutoka mashariki na kufikia Jiayuguan upande wa magharibi, jumla una urefu wa kilomita 5660, na kipande cha ukuta huo cha Badaling kiungani mwa Beijing kina thamani kubwa katika sanaa.