Majengo ya Enzi ya Qing

中国国际广播电台

       Enzi ya Qing (1616-1911) ni enzi ya mwisho ya kifalme nchini China. Majengo katika enzi hiyo mengi zaidi yalirithi mtindo wa enzi iliyotangulia ya Ming ingawa yalitokea mabadiliko kidogo ya kufanya majengo yawe ya kifahari zaidi.
Mji wa Beijing katika enzi hiyo ulikuwa sawa na enzi ya Ming. Kwenye kuta za mji kuna malango 20 na ndani ya mji kuna makasri makubwa. Katika enzi hiyo bustani nyingi za kifalme zilijengwa, kati ya bustani hizo zilizo kubwa na maarufu ni bustani ya Yuan Ming Yuan na kasri la majira ya joto (Summer Palace).