中国国际广播电台
Majengo ya kisasa yanamaanisha
majengo yaliyojengwa kuanzia
katikati ya karne ya 19 hadi
sasa.
Tokea vita vya kasumba vya
mwaka 1840 hadi Jamhuri ya
Watu wa China kuasisiwa mwaka
1949, majengo yenye mtindo
wa Kichina na wa Kimagharibi
yalitokea nchini China. Katika
kipindi hiki majengo ya mtindo
wa Kichina yanaendelea kuwa
mengi, lakini nyumba za michezo,
mahoteli, maduka, na maduka
makubwa yalikuwa hujengwa
kwa mchanganyiko wa mitindo
ya Kichina na ya Kimagharibi
na majengo ya aina ya Kimagharibi
yalitokea katika miji ya Shanghai,
Tianjin, Qingdao na Harbin
kwenye sehemu zilizokodiwa
na nchi za nje, na pia majengo
ya ubalozi, benki za nchi
za nje na mahoteli na klabu
za nchi za nje zilitokea katika
miji hiyo.
Baada ya Jamhuri ya Watu
wa China kuasisiwa mwaka 1949,
ujenzi umeingia katika kipindi
kipya cha kihistoria, kutokana
na jinsi uchumi ulivyoendelea
kwa haraka ujenzi wa majengo
uliongezeka. Katika kipindi
hiki majengo makubwa 10 yenye
mapaa ya aina ya kasri la
kifalme yalijengwa katika
mwaka wa maadhimisho ya miaka
kumi tokea Jamhuri ya Watu
wa China iasisiwe. Tokea miaka
ya 80 ya karne iliyopita,
majengo yameanza kuwa na aina
kwa aina.
|