Wasanifu majengo Wakubwsa wa China
中国国际广播电台

 Liang Sicheng

      Liang Sicheng (1901—1972), mwaka 1915 hadi 1923 alisoma katika Chuo Kikuu cha Qinghua mjini Beijing, mwaka 1927 alipata shahada ya pili na mwaka 1948 alipata shahada ya daktari katika chuo kikuu kimoja cha Marekani. Maishani mwake alitoa mchango mkubwa katika elimu na majengo.

Liang Sicheng alianza kutafiti majengo ya kale ya China katika miaka ya 30 ya karne iliyopita na aliandika makala nyingi zenye thamani kubwa kuhusu utaalamu wa majengo ya kale ya China.

Liang Sicheng alitoa mashauri mengi kuhusu mpangilio wa majengo ya mji wa Beijing, aliwahi kushiriki kazi ya kusanifu nembo ya taifa na mnara wa mashujaa wa China katika uwanja wa Tian An Men.

Liang Sicheng alikuwa mmoja wa watangulizi waliofanya utafiti wa majengo ya kale ya China, makala zake za utafiti zina thamani kubwa katika nyanja ya ujenzi.



Wu Liangyong

       Wu Liangyong alizaliwa mwaka 1922, aliwahi kuwa mwenyekiti wa Shirikisho la Kimataifa la Ujenzi (UIA) na mwenyekiti wa Shirika la Makazi ya Dunia (WSE). Aliwahi kutoa mashauri mengi kuhusu majengo ya Kichina na mpangilio ya majengo ya miji. Usanifu wake wa nyumba zenye ua wa mraba katika kichochoro cha Ju Er mjini Beijing ulipata tuzo ya Shirika la Makazi ya Binadamu la Umoja wa Mataifa mwaka 1992, na mwaka 1993 alitoa sayasi ya mazingira ya makazi ya binadamu, na mwaka 1996 alipata tuzo ya Shirikisho la Wasanifu Majengo la Kimataifa.


Zhang Kaiji

     Zhang Kaiji ni msanifu majengo wa awamu ya kwanza baada ya Jamhuri ya Watu wa China kuasisiwa. Alizaliwa mwaka 1912 mjini Shanghai, na mwaka 1935 alihitimu katika Chuo Kikuu cha Nanjing, aliwahi kuwa msanifu mkuu majengo katika taasisi ya usanifu majengo ya Beijing na naibu mkurugenzi wa bodi ya Shirikisho la Wasanifu Majengo la China, na mwaka 1990 alipata sifa ya “Msanifu mkuu wa Majengo”, mwaka 2000 alipata “tuzo ya Majengo ya Liang Sicheng”. Aliwahi kusanifu jukwaa la kuangalia gwaride katika uwanja wa Tian An Men, jumba la makubusho ya mapinduzi ya China na jumba la makubusho ya historia ya China, jumba la wageni wa kitaifa na jumba la unajimu la Beijing.


 

 

Yang Tingbao

Yang Tingbao (1901—1982), alihitimu katika Chuo Kikuu cha Qinghua mjini Beijing, na alibakizwa kuwa mwalimu katika chuo chake na wakati huo alitumwa na chuo chake kwenda Marekani kuendeleza zaidi masomo. Alipokuwa Marekani alipata tuzo ya kwanza katika mashindano ya usanifu ya Emerson (Emerson Prize Competition) mwaka 1924, na mwaka huo pia alipata tuzo ya kwanza ya mashindano ya Shirikisho la Sanaa ya Manispaa (Municipal Art Society Prize Competition).

Tokea mwishoni mwa miaka ya 20 ya karne iliyopita, aliwahi kusanifu benki ya mawasiliano ya Beijing, hospitali kuu ya Nanjing, maktaba ya Chuo Kikuu cha Qinghua, Chuo Kikuu cha Shenyang, Hoteli ya Amani ya Beijing, na pia aliwahi kushiriki katika usanifu wa ukumbi mkuu wa umma mjini Beijing, kituo cha garimoshi cha Beijing, maktaba ya Beijing na ukumbi wa kumbukumbu ya Mwenyekiti Mao mjini Beijing. Majengo yake yalitiliwa mkazo muunganisho wa mitindo ya Kichina na ya kimagharibi.