Elimu ya Sekondari ya Chini
Radio China Kimataifa

Elimu ya sekondari ya chini nchini China pia ni elimu ya lazima, inatumia miaka mitatu. Masomo yanayofundishwa ni Kichina, hisabati, lugha za kigeni, fizikia, kemikali, maadili, upashanaji habari na kadhalika. Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa hivi karibuni, China ina shule zaidi ya elfu 60 za sekondari ya chini zenye wanafunzi milioni 60, ambao wanachukua asilimia 90 na zaidi ya idadi ya watoto wanaotimiza umri wa kwenda shule ya sekondari. Shule nyingi kabisa za sekondari ya chini zinaendeshwa na serikali.

Kwa kuwa elimu ya sekondari ya chini ni elimu ya lazima, hivyo wanafunzi hawana haja ya kufanya mtihani wa kujiunga na sekondari ya chini, wanaweza kuchagua shule kutokana na mahali wanakoishi na matakwa yao yenyewe. Katika sehemu za vijijini, wanafunzi wanapelekwa katika shule zenye hali nzuri zaidi, wanalala shuleni. Hivi sasa China inajitahidi kukuza elimu kwa kupitia mtandao wa kompyuta ili kutimiza lengo la kutumia pamoja vyanzo vya elimu vya sehemu mbalimbali.