Elimu ya Juu
Radio China Kimataifa

Elimu ya juu ya China imegawanyika kuwa elimu ya vyuo vya diploma, elimu ya vyuo vikuu, na mafunzo ya shahada ya pili na ya udaktari. Kuna vyuo vikuu, vyuo vya ufundi, vyuo vikuu vinavyotoa mafunzo kwa njia ya televisheni na radio, na vyuo vikuu vya watu wazima.

Elimu ya juu nchini China ina historia zaidi ya miaka mia moja. Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa hivi karibuni, China ina vyuo vikuu 3000 vya aina mbalimbali, ambapo theluthi mbili vinaendeshwa na serikali, na theluthi moja vinaendeshwa na watu binafsi. Kuna wanafunzi milioni 20 wa vyuo vikuu, ambao wanachukua asilimia 17 ya idadi ya Wachina wa rika moja.

Nchini China wanafunzi wanatakiwa kufanya mtihani wa kujiunga na chuo kikuu, vyuo vikuu vinawaandikisha wanafunzi kutokana na matakwa yao na matokeo yao ya mtihani.

Katika miaka miwili iliyopita, idara za elimu za China zinafanya juhudi kukuza elimu ya juu, ambapo vyuo vikuu vya serikali vimeongeza kuwaandikisha wanafunzi, na elimu ya shahada ya pili na ya udaktari pia imepata maendeleo mazuri.