Mhitani wa Kujiunga na Sekondari ya Juu
Radio China Kimataifa

Nchini China wanafunzi wanapaswa kufanya mtihani wa kujiunga na sekondari ya juu baada ya kumaliza masomo ya sekondari ya chini. Kwa kuwa ni asilimia 60 tu ya wanafunzi wanaomaliza masomo ya sekondari ya chini wanaweza kuendelea na masomo ya sekondari ya juu, kiasi hicho hata ni chini ya kile cha wanafunzi wanaohitimu sekondari ya juu kujiunga na chuo kikuu, hivyo mtihani huo ni mmoja wa mitihani migumu kabisa nchini China.

Mtihani wa kujiunga na sekondari ya juu hutolewa na idara za elimu za sehemu mbalimbali. Masomo ya mtihani huwa ni Kichina, lugha ya kigeni, hisabati, fizikia na kemia. Mtihani hufanyika mwezi wa Juni kila mwaka.

Wanafunzi hawawezi kujiunga na katika sekondari ya juu bila kuwa na matokeo mazuri katika mtihani huo, halafu watapata fursa ya kujiunga na chuo kikuu, na kuwa na mustakabali mzuri wa kupata ajira bora. Kama wakishindwa katika mtihani huo, basi hawawezi kusoma katika sekondari ya juu, na wataanza kufanya kazi wakiwa na hali duni ya elimu. Kwa hivyo Wachina wengi wanaona kuwa mtihani huo unaamua mustakabali wa maisha ya watoto.