Mtihani wa Kujiunga na Chuo Kikuu
Radio China Kimataifa

Mtihani huo hutolewa na idara za kitaifa au kimkoa kutokana na maelekezo ya muongozo wa mtihani unaotolewa na wizara ya elimu ya China. Mtihani huo unaofanyika kwa siku mbili au tatu, huanzia tarehe 7 Juni ya kila mwaka.

Hivi sasa, mambo yaliyomo katika mtihani wa kujiunga na chuo kikuu ni "3+X", 3 inamaanisha Kichina, hisabati na lugha ya kigeni, "X" inaweza kuwa mtihani wa masomo tofauti katika mitihani tofauti ya kitaifa na kimkoa. Katika baadhi ya sehemu "X" inawakilisha mtihani wa mseto wa sanaa na sayansi. Baadhi ya sehemu "X" inawakilisha masomo ya fizikia, kemia, biolojia, historia na kadhalika wanafunzi wanaochagua wenyewe.

Mtihani wa kujiunga na chuo kikuu unafuatiliwa sana na jamii ya China, lakini katika miaka ya hivi karibuni, kutokana na vyuo vikuu kuongeza wanafunzi, shinikizo la watahiniwa na wazazi limepungua kidogo.