Mtihani wa Shahada ya Pili na ya Udaktari
Radio China Kimataifa

Mtihani wa shahada ya pili nchini China hugawanya katika sehemu mbili ya mtihani wa maandishi na mtihani wa maongezi. Mtihani wa maandishi wa kozi za kawaida hutolewa na wizara ya elimu ya China, na kupanga maksi za chini kabisa za kuandikisha watahiniwa, kwa mfano watahiniwa wa kozi za fani hiyo wanatakiwa kufanya mtihani wa siasa na lugha ya kigeni, ambapo watahiniwa wa sayansi lazima wafanye mtihani wa siasa, lugha ya kigeni na hisabati. Mtihani wa somo maalum huamuliwa na vyuo vikuu au mashirika ya utafiti. Watahiniwa wakifikia maksi zinazokubalika, basi wataendelea kufanya mtihani wa maongezi. Vyuo vikuu na mashirika ya utafiti yatawaandikisha watahiniwa kutokana na matokeo yao katika mtihani wa maandishi na maongezi.

Mtihani wa shahada ya udaktari hutolewa na vyuo vikuu au mashirika ya utafiti yanayowaandikisha wanafunzi. Watahiniwa wa shahada ya pili wakitaka kuendelea na masomo ya shahada ya udaktari ya kozi wanayojifunza, basi wanatakiwa tu kufanya mtihani wa maandishi na maongezi ya lugha ya kigeni na masomo mengine mawili au tatu. Ama sivyo wanatakiwa kufanya mtihani wa maandishi na maongezi ya masomo matano au sita.

Katika miaka ya hivi karibuni, kutokana na shinikizo la kupata ajira, idadi ya watahiniwa wanaofanya mtihani wa shahada ya pili na ya udaktari imeongezeka kwa haraka. Isitoshe, kutokana na mageuzi ya mfumo wa elimu, mashirika yanayowaandikisha wanafunzi yana haki zaidi ya kujiamulia katika mtihani.