Chuo Kikuu cha Beijing
Radio China Kimataifa


Chuo Kikuu cha Beijing ni chuo kikuu cha elimu za mseto cha kitaifa ambacho kinajulikana nchini kutokana na kiwango kikubwa cha utoaji elimu na utafiti. Chuo hicho ilianzishwa mwaka 1898, ni kimoja cha vyuo vikuu vyenye historia ndefu nchini China.

Baada ya maendeleo ya miaka mia moja, hivi sasa Chuo Kikuu cha Beijing kina sehemu tano za utamaduni, sayansi ya jamii, sayansi, upashanaji habari na uhandisi na utibabu. Kina tovuti 42, vituo 216 vya utafiti, na hospitali 18 za kufundishia zilizo chini yake. Kozi za chuo kikuu hicho za Kichina, lugha za kigeni, historia, fizikia na viumbe zinajulikana zaidi nchini China.

Chuo Kikuu cha Beijing sasa kina wanafunzi zaidi ya elfu 15 wa shahada ya kwanza, na wanafunzi elfu 12 wa shahada ya pili na ya udaktari, pia kimewavutia wanafunzi wengi wa nchi za nje. Maktaba ya Chuo Kikuu cha Beijing ni maktaba kubwa kabisa cha chuo kikuu katika bara la Asia, ina vitabu milioni 6.29. Kama ukitaka kufahamu habari nyingi zaidi kuhusu Chuo Kikuu cha Beijing, soma tovuti ya chuo hicho : http://www.pku.edu.cn/