Chuo Kikuu cha Ualimu cha Beijing  
中国国际广播电台


      Chuo Kikuu cha Ualimu cha Beijing kilianzishwa mwaka 1902, ni chuo kikuu cha kwanza cha ualimu katika historia ya China, na pia ni chuo kikuu maarufu kati ya vyuo vya ualimu nchini China.

Katika chuo kikuu hicho kuna chuo cha elimu, chuo cha kuwaandaa walimu, chuo cha lugha ya Kichina na vyuo vingine vipatavyo 15 kwa jumla vyenye masomo 48. kati ya masomo hayo somo la elimu, saikolojia, elimu kabla shule ya msingi zinajulikana zaidi.

Katika chuo kikuu hicho kuna wafanyakazi na walimu karibu 2500, wanafunzi zadi ya elfu 20, na wanafunzi kutoka nchi za nje 1000.

Katika miaka ya karibuni licha ya kuendeleza masomo ya ualimu, chuo kikuu hicho kimestawisha zaidi masomo mengine yasiyo ya ualimu, pia kimeanzisha mafunzo ya kuwapatia walimu wa kazini ujuzi zaidi.

http://www.bnu.edu.cn/