Chuo Kikuu cha Nanjing
Radio China Kimataifa


Chuo Kikuu cha Nanjing kiko katika mji wa Nanjing, mji mkuu wa mkoa wa Jiangsu, kinajulikana zaidi kwa kozi za sayansi na uhandisi, na ni moja ya vyuo vikuu maarufu nchini China.

Hivi sasa Chuo Kikuu cha Nanjing kina vitivo 43 katika taasisi 16 ambavyo ni pamoja na chuo cha fasihi, chuo cha sayansi, chuo cha jiografia na chuo cha utibabu, kina walimu 2000 na wanafunzi elfu 31, miongoni mwa wanafunzi hao, wanafunzi zaidi ya 8500 wanasomea shahada ya pili na ya udaktari.

Chuo Kikuu cha Nanjing ni moja ya vyuo vikuu vinavyofanya shughuli nyingi za maingiliano ya taaluma ya kimataifa. Maprofesa wengi waliopata tuzo ya Nobel wakiwemo Li Zhengdao, Ting Zhaozhong, Yang Zhenning, Glashow, Robert A. Mundell wamekuwa maprofesa wa heshima wa Chuo Kikuu cha Nanjing. Kama ukitaka kufahamu habari nyingi zaidi kuhusu Chuo Kikuu cha Nanjing, soma tovuti:http://www.nju.edu.cn/