Chuo Kikuu cha Sichuan
Radio China Kimataifa


Chuo Kikuu cha Sichuan kiko mjini Chengdu, mji mkuu wa mkoa wa Sichuan, kusini magharibi mwa China, hiki ni chuo kikuu chenye kozi nyingi na kiwango kikubwa katika sehemu ya kusini magharibi ya China. Hivi sasa, kinatoa mafunzo yanayohusiana na sekta 9 za utamaduni, sayansi ya jamii na maumbile, uhandisi na utibabu.

Hivi sasa Chuo Kikuu cha Sichuan kina vitivo 30 vyenye kozi 118, kina walimu na wafanyakazi 11,357 na wanafunzi elfu 43.9, kati yao wanafunzi 10,000 wanasomea shahada ya pili na 2,740 wanasomea shahada ya udaktari, na wanafunzi 653 wanatoka nchi za nje na sehemu ya Macao na Hongkong. Ukitaka kufahamu habari nyingi zaidi kuhusu chuo kikuu hicho, soma tovuti yake: http://www.scu.edu.cn/