Mikataba ya kimataifa ya mazingira ambayo China imeasini

Radio China Kimataifa
 

China ikiwa na msimamo wa kuwajibika na juhudi za hifadhi ya mazingira na maliasili duniani, imejiunga au kusaini mikataba na makubaliano ya kimataifa zaidi ya 30 kuhusu hifadhi ya mazingira na maliasili. Mikataba hiyo ni kama ifuatayo:

"Mkataba wa kimataifa wa kuzuia uchafuzi wa mafuta baharini" (mwaka 1954, London)

"Mkataba kuhusu kuvua samaki na kutunza maliasili ya viumbe baharini" (mwaka 1958, Geneva)

"Mkataba wa kimataifa wa usimamizi wa shughuli za kuvua pomboo" (Mwaka 1946, Washington)

"Mkataba wa Asia ya kusini mashariki kuhusu hifadhi ya mimea" (mwaka 1956, Rome)

"Mkataba kuhusu sehemu ya rasi" (mwaka 1958, Geneva)

"Mkataba wa ncha ya kusini" (mwaka 1959, Washington)

"Mkataba wa jumuiya ya hali ya hewa duniani" (mwaka 1947,Washington)

"Mkataba wa kimataifa kuhusu wajibu wa mambo ya kiraia juu ya uchafuzi wa mafuta duniani" (mwaka 1969, Brussers)

"Mkataba wa hifadhi ya mali za urithi za utamaduni na maumbile duniani" (mwaka 1972, Paris)

"Mkataba kuhusu kanuni zinazopaswa kufuatwa na nchi mbalimbali katika kufanya utafiti na kutumia nafasi za anga ya juu pamoja na mwezi na sayari nyingine" (mwaka 1972, Moscow)

"Mkataba wa kuzuia uchafuzi baharini kutokana na kutupa takataka na vitu vingine" (mwaka 1972, London)

"Mkataba kuhusu kupiga marufuku kuendeleza, kutengeneza na kulimbikiza vijidudu (viumbe) na silaha zenye sumu na kuteketeza silaha kama hizo" (mwaka 1972, London)

"Mabakuliano kuhusu kufanya mawasiliano kwenye bahari za kimataifa wakati uchafuzi unaosababishwa na vitu visivyo vya mafuta" (mwaka 1973, London)

"Mkataba wa kimataifa wa kuzuia uchafuzi unaosababishwa na meli" (mwaka 1978, London)

"Mkataba wa hifadhi ya vifaa na vitu halisi vya kinyuklia" (mwaka 1979, Viena)

"Mtakaba wa Vienna wa hifadhi ya ukanda wa ozone" (mwaka 1985, Viena)

"Mkataba kuhusu utoaji msaada wakati wa kutokea kwa tukio la dharura la kinyuklia au la mionzi ya x-ray" (mwaka 1985, Viena)

"Mkataba kuhusu tukio la kinyuklia na utoaji ripoti mapema" (mwaka 1985,Vienna)

"Mkataba wa Montreal kuhusu vitu vya kudhoofisha tabaka la ozone" (mwaka 1987, Montreal)

"Mkataba wa mfumo wa kituo cha ufugaji wa samaki wa Asia na Pasifiki" (mwaka 1988, Bangkok)

"Mkataba wa Basel kuhusu kudhibiti uhamishaji wa takataka zenye hatari kwa nchi za nje na kushughulikia takataka hizo" (mwaka 1989, Basel)

"Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa" (Mwaka 1992, Rio de Janeiro)

"Mkataba kuhusu aina nyingi za viumbe" (mwaka 1992, Rio de Janeiro)

"Mkataba wa Serikali za Jamhuri ya Watu wa China na Shirikisho la Jamhuri za kisoshalisti za kisoviet kuhusu ulindaji wa pamoja wa misitu na kukinga moto" (mwaka 1980)

"Mkataba wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na Serikali ya Japan kuhusu kulinda ndege wanaohamahama na mazingira yao ya kuishi" (mwaka 1981)

"Mkataba wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na Serikali ya Australia kuhusu kulinda ndege wanaohamahama na mazingira yao ya kuishi" (mwaka 1986)

"Mkataba wa Jamhuri ya Watu wa China na Jamhuri ya kiislamu ya Pakistan kuhusu ushirikiano wa matumizi ya kiamani ya nishati ya nyuklia" (Mwaka 1986)

Zaidi ya hayo, China pia imefanya juhudi za kuunga mkono nyaraka nyingi muhimu kuhusu hifadhi ya mazingira na maliasili za kimataifa, na kuingiza moyo wa nyaraka hizo kwenye sheria na sera za China. Nyaraka hizo ni pamoja na "Taarifa ya Umoja wa Mataifa kuhusu mazingira ya binadamu" iliyotolewa mwaka 1972 huko Stockholm, Sweden, "Mwongozo mkuu wa hifadhi ya maliasili za dunia" uliotolewa mwaka 1980 na nchi nyingi duniani kwa wakati mmoja, "Taarifa ya Nairobi" iliyotolewa mwaka 1982 huko Nairobi, Kenya na "Taarifa ya Rio de Janeiro kuhusu mazingira na maendeleo" iliyotolewa mwaka 1992 huko Rio de Janeiro, Brazil.