China na "Mkataba wa Montreal"

Radio China Kimataifa
 

Katika miaka 10 iliyopita, China imeshiriki kwa juhudi katika shughuli mbalimbali za kimataifa za kulinda tabaka la ozone. Mwaka 1986, 1987 China iliwatuma wajumbe kuhudhuria mkutano wa kikundi cha kulinda ngazi ya ozone na mkutano wa kusaini "barua ya makubaliano". Mwaka 1989 China ilijiunga rasmi na mkataba huo, na kwenye mkutano wa kwanza wa nchi zilizosaini mkataba, China ilitangulia kutoa pendekezo kuhusu "kuanzisha mfuko wa pande nyingi wa kulinga ngazi ya ozone". Mwaka 1990, China ilishirikiana na nchi mbalimbali duniani katika juhudi za kushiriki kwenye kazi ya marekebisho ya "Waraka wa makubaliano". Mwaka 1991, China ilijiunga rasmi na mswada wa marekebisho wa London kuhusu "Waraka wa makubaliano", na ilianzisha kwa wakati ofisi ya kikundi cha uongozi cha China cha kulinda ngazi ya ozone kilichoshirikisha wizara, kamati, makampuni makuu na mashirikiano makuu ya China yapatayo 15, ili kubeba kazi ya utekelezaji wa waraka huo wa makubaliano. Mwaka 1992, China ilitangulia kutunga "Mpango wa nchi ya China wa kuchuja hatua kwa hatua vitu vya kudhoofisha ozone", na mpango huo uliidhinishwa mwanzoni mwa mwaka 1993 na Baraza la serikalli na Kamati ya utendaji wa mfuko wa pande nyingi. Mwaka 1994, China ilitunga "Nyongeza za mpango wa mashirika ya tumbaku kuchuja hatua kwa hatua vitu vya kudhoofisha ozone".

Mpaka hivi sasa kupitia Benki ya dunia, Shirika la mipango ya maendeleo la Umoja wa Mataifa, Shirika la viwanda na maendeleo la Umoja wa Mataifa, na Shirika la mipango ya mazingira la Umoja wa Mataifa, pamoja na nchi za Marekani, Canada, Ujerumani na Denmark, miradi 156 ya China imeidhinishwa na Kamati ya utendaji ya Mfuko wa pande nyingi, na kupata dola za kimarekani milioni 105. Kama miradi hiyo yote itakamilika, vitu vinavyodhibitiwa vitapungua kwa tani elfu 31.8.