China yapanga kujenga nchi yenye majumba ya makumbusho mengi zaidi ifikapo mwaka 2035
2021-05-24 20:08:38| CRI

Ili kuhimiza maendeleo yenye sifa bora ya mambo ya majumba ya makumbusho ya China, idara 9 za China zimetangaza mwongozo wa kuhimiza mageuzi na maendeleo ya majumba ya makumbusho.

Mwongozo huo unasema, ifikapo mwaka 2035 utaratibu wa jumba la makumbusho wenye umaalumu wa China utapevuka zaidi, uwezo wa kijamii wa jumba la makumbusho utaimarishwa, na kujenga nchi yenye majumba ya makumbusho mengi zaidi duniani, na kutoa busara ya China na mpango wa China kwa ajili ya maendeleo ya majumba ya makumbusho duniani.