Marais wa Russia na Marekani kukutana tarehe 16 Juni
2021-05-26 19:11:33| CRI

Habari kutoka tovuti ya rais ya Russia leo zinasema, rais Vladmir Putin wa Russia na mwenzake Joe Biden wa Marekani watakutana mjini Geneva, Uswis mnamo tarehe 16 Juni.

Habari zinasema kuwa, marais hao wawili watajadiliana hali ya sasa ya uhusiano kati ya nchi hizo mbili na mustakabali wake, utulivu wa kimkakati, ushirikiano kuhusu mapambano dhidi ya COVID-19 na kusuluhisha mgogoro wa kikanda.