Pendekezo la Ukanda Mmoja, Njia Moja laendana na mwelekeo wa maendeleo wa Ajenda ya 2063 ya Umoja wa Afrika
2021-12-20 09:09:37| CRI

Pendekezo la Ukanda Mmoja, Njia Moja laendana na mwelekeo wa maendeleo wa Ajenda ya 2063 ya Umoja wa Afrika_fororder_African Union Commission Deputy Chairperson Erastu

Naibu mwenyekiti wa zamani wa Kamati ya Umoja wa Afrika, Erastus Mwencha amesema, pendekezo la Ukanda Mmoja, Njia Moja linaendana na ajenda ya maendeleo ya mwaka 2063 ya Umoja huo, na linaharakisha uboreshaji wa miundombinu na muungano wa soko barani Afrika.

Mwencha amesema, pendekezo hilo linafuata maslahi ya maendeleo ya Afrika, na litaleta teknolojia na mitaji kwa Afrika katika kuendeleza uchumi wa kidijitali, kuongeza uwezo wa uzalishaji bidhaa, kuhimiza uhamishaji wa teknolojia, kuhamasisha uwekezaji kwa sekta zisizosababisha uchafuzi, na kukuza mawasiliano ya watu na utamaduni.

Amesema, utekelezaji wa mfululizo wa miradi ya Ukanda Mmoja, Njia Moja, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa barabara, reli, bandari, na miundombinu ya kidijitali, umebadilisha sura ya Afrika kuboresha  maisha ya watu barani humo.