Wahisani wachina watoa matumaini kwa vijana wanafunzi kwenye makazi ya mabanda nchini Kenya
2022-06-13 08:39:11| CRI

Wahisani wachina wanaendelea kuwapa matumaini wanafunzi vijana wanaosoma kwenye shule ya Mcedo Beijing iliyopo kwenye eneo la makazi ya mabandaduni la Mathare mjini Nairobi.

Watoto hao wanaotoka kwenye mazingira magumu wamejiunga na shule hiyo kutokana na hisani ya wachina na sasa wanaweza kukata kiu yao ya elimu.

Wanafunzi hao wanasema kabla ya hisani kutoka kwa wachina, madarasa ya shule hiyo yalikuwa ni ya muda, lakini sasa wana majengo ya kudumu yanayofanya wasome kwa furaha.

Shule ya Mcedo Beijing ilianza kujengwa mwaka 2007 kwa msaada wa ubalozi wa China, na baadaye jumuiya ya uchumi na biashara ya China na Kenya iliyahamasisha makampuni wanachama ya China kukusanya fedha na kuipanua shule hiyo.