Siku ya Taasisi ya Confucius Duniani yasherehekewa Tunisia
2022-09-28 09:38:32| CRI

Taasisi ya Confucius ya Tunisia imesherehekea Siku ya Taasisi ya Confucius Duniani Jumanne wiki hii huko Tunis.

Mkurugenzi wa taasisi hiyo Bw. Ding Yang, alipohutubia sherehe hiyo alisema siku hiyo inaonyesha thamani kubwa na sifa ya kipekee ya utamaduni na ustaarabu wa China, na huu ni wakati unaofaa kwa watu wa China na watu wa nchi mbalimbali duniani kuunganisha staarabu zao.

Mkurugenzi wa Idara ya lugha za Mashariki ya Chuo Kikuu cha Carthage Bw. Khaled Haj Ahmed ameliambia shirika la habari la Xinhua kwamba mamia ya wanafunzi wa Tunisia wanajifunza lugha ya Kichina, na kampuni nyingi za China nchini Tunisia zikitaka kuajiri wenyeji wenye ujuzi na wenye diploma ya lugha ya Kichina.

Taasisi ya kwanza ya Confucius nchini Tunisia iliyojulikana kama Taasisi ya Lugha na Utamaduni wa China ilianzishwa mwezi Novemba mwaka 2018.