Kenya yaharakisha kuzuia kukua kwa deni la nje wakati thamani ya fedha ya nchi hiyo ikishuka
2022-10-13 08:23:49| CRI

Kenya inachukua hatua ya kutuliza sarafu yake katika deni la nje ili kuzuia ukuaji wa kasi wa deni hilo kufuatia sarafu ya nchi hiyo kushuka thamani dhidi ya sarafu kubwa za kimataifa.

Kwa mujibu wa Hazina ya Taifa nchini humo, shilingi ya Kenya imeshuka kwa karibu asilimia 8 dhidi ya dola ya kimarekani ikilinganishwa na mwaka jana kipindi kama hicho.