Serikali ya Somalia imesema imeanza uchunguzi kuhusu mashambulizi ya anga yaliyotokea hivi karibuni ambayo yameteketeza minara ya mawasiliano ya simu na kudhoofisha shughuli za Kampuni mawasiliano ya simu ya Hormuud Telecom, ambayo ni kampuni kubwa zaidi ya mawasiliano nchini humo.
Wizara ya Ulinzi imelaani mashambulizi hayo yaliyotokea huko Jubba na Gedi ambayo yalitekelezwa Jumanne katika eneo la Jilib ambalo ni ngome ya kundi la al-Shabaab katika eneo la Juba ya Kati. Hali halisi ya mashambulizi hayo bado haijajulikana.
Wizara hiyo imesema inawasiliana moja kwa moja na Tume ya Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM na washirika wengine wanaotoa msaada kwa serikali hiyo katika operesheni za usalama ili kueleza wasiwasi wake na kujua kilichotokea katika maeneo hayo.