Mwanamichezo kutoka Madagascar Mialitiana CLERC afurahia kushiriki Michezo ya Olimpiki ya Majira Baridi Beijing
2022-02-21 08:21:05| CRI

Mwanamichezo kutoka Madagascar Mialitiana CLERC ni mmoja wa wanamichezo sita kutoka nchi tano za Afrika walioshiriki kwenye Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing, na pia ni mwanamichezo wa kwanza mwanamke kuiwakilisha Madagascar kushiriki kwenye michezo hiyo.

Hii ni mara yake ya pili kushiriki Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi na nafasi yake kwenye mashindano ya Women's Giant Slalom imepanda kutoka 48 mwaka 2008 hadi 41 hapa Beijing.

Akihojiwa hivi karibuni na Shirika Kuu la Utangazaji la China CMG, Bibi Mialitiana amesema anatumai kwamba uzoefu wake utawahamasisha watu wote wa Afrika, hasa wanawake kuwa na uthubutu wa kufuata ndoto zao kama alivyofanya yeye, na kufurahia maisha kwa tabasamu.

Mwanamichezo kutoka Madagascar Mialitiana CLERC afurahia kushiriki Michezo ya Olimpiki ya Majira Baridi Beijing_fororder_IMG-20220216-WA0004

Mwanamichezo kutoka Madagascar Mialitiana CLERC afurahia kushiriki Michezo ya Olimpiki ya Majira Baridi Beijing_fororder_IMG-20220216-WA0002

Mwanamichezo kutoka Madagascar Mialitiana CLERC afurahia kushiriki Michezo ya Olimpiki ya Majira Baridi Beijing_fororder_IMG-20220216-WA0005