Idadi ya watu waliofariki katika mlipuko uliotokea jumatatu wiki hii katika mgodi wa dhahabu kusini magharibi mwa Burkina Faso imeongezeka na kufikia 63.
Gavana wa mkoa wa Kusini-Magharibi, Emmanuel Zongo amesema, mgodi huo umefungwa mpaka itakapotangazwa tena.
Chanzo cha mlipuko huo bado hakijafahamika, na uchunguzi unaendelea.