Waziri wa Mambo ya Nje wa China Bw. Wang Yi amesema Akili Mnemba (AI) haipaswi kutumiwa kama chombo cha kudumisha umwamba.
Bw. Wang ametoa kauli hiyo kwenye Mkutano wa ngazi ya juu wa Ushirikiano wa Kimataifa kuhusu Kujenga Uwezo wa mambo ya Akili Mnemba kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York.
Amesema China inazingatia maendeleo ya Akili Mnemba kwa manufaa ya watu na kuepuka matumizi mabaya ya teknolojia hiyo.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Bw. Lin Jian amewaambia wanahabari kuwa, kwenye mkutano huo China ilitangaza Mpango wa Utekelezaji wa Uwezo wa AI kwa Wema na kwa ajili ya Wote. Mpango huo unalenga kupunguza migawanyiko na kuhimza utekelezaji wa Ajenda ya Umoja wa Mataifa ya 2030 ya Maendeleo Endelevu.
Mapendekezo matano yalitolewa kwenye maeneo ya ushirikiano yanayokidhi matarajio ya pande zote, hasa nchi za Kusini, ambayo ni miundombinu ya AI, uwezeshaji wa viwanda, mafunzo ya wafanyakazi, maendeleo ya data na usimamizi wa wa usalama.