6: Makabila na Dini

Makabila ya China

China ni nchi yenye makabila mengi, ina idadi kubwa kabisa ya watu duniani. Hivi sasa China ina watu bilioni 1.3 na makabila 56.

Makabila ya China ni kama yafuatayo: wahan, wamongolia, wahui, watibet, wauigur, wamiao, wayi, wazhuang, wabuyi, wakorea, waman, watong, wayao, wabai, watujia, wahani, wakazakstan, wadai, wali, walisu, wa-wa, washe, wagaoshan, walahu, washui, wadongxiang, wanaxi, wajingpo, wakhalkhas, wa-tu, wadawoer, wamulam, waqiang, wabulang, washala, wamaonan, wagelao, waxibo, waachang, wapumi, watajik, wa-nu, wauzbek, warussia, waewenk, wadeang, wabaoan, wayugu, wajing, watataer, wadulong, waelunchun, wahezhe, wamenba, waluoba na wakinuo. Zaidi ya hayo, nchini China pia kuna watu wasiojulikana wa kabila gani.

Nchini China, watu wa kabila la Han wanachukua takriban asilimia 92 ya idadi ya wachina wote, ambapo watu kutoka kwenye makabila madogo 55 wanachukua asilimia 8. Kwa kuwa idadi ya watu wa makabila mengine 55 ni ndogo , hivyo huitwa makabila madogo. Makabila mengi madogo yanakaa katika sehemu ya kaskazini magharibi, kusini magharibi na kaskazini mashariki mwa China.

Kutokana na maendeleo ya historia ndefu ya China, watu wa kabila la Han na baadhi ya makabila madogo wanaishi kwa kuchanganyika,ambapo watu wengine wa makabila madogo wanakaa katika sehemu ndogo. Licha ya kabila la Hui na kabila la Man yanayotumia lugha ya Han, yaani lugha ya taifa la China, makabila mengine madogo yote yana lugha zao zenyewe huku wakitumialugha ya Kichina. Katika miaka mingi iliyopita, watu wa makabila 56 wa China walikuwa wakifanya kazi na kuishi pamoja kwenye eneo lenye kilomita za mraba milioni 9.6, na kukuza kwa pamoja ustaarabu wenye historia ndefu.

Makabila Yenye Watu Zaidi ya Milioni Tano

Kabila la Han

Kabila la Han ni kabila lenye idadi kubwa kabisa la watu nchini China hata duniani. Hivi sasa lina watu bilioni 1.2. Watu wa kabila la Han walikuwa wakazi wa sehemu ya katikati ya China, ambao waliitwa "huaxia", wamekuwa na ustaarabu wenye historia ya miaka 5000. Baadaye waliishi pamoja na makabila mengine. Kuanzia enzi ya Han, watu wa "huaxia" walianza kuitwa rasmi kuwa kabila la "Han", lilikuwa na lugha na maandishi yake yenyewe, yaani Kichina. Kichina ni lugha ya mfumo wa "Han-Tibet", hugawanyika kuwa lahaja aina nane za kienyeji, yaani kaskazini, Wu, Xiang, Gan, Kejia, Minnan, Minbei na Yue. Kichina sanifu pia kinaitwa "Mandrine", Kichina ni moja ya lugha zenye historia ndefu zaidi duniani, maandishi yake yaliendeleza taratibu kutoka maandishi yaliyoandikwa kwenye mifupa au magamba ya kobe, au shaba nyeusi hadi herufi za Kichina za sasa (Chinese characters), Kichina kina maneno zaidi ya elfu 80, kati yao maneno 7000 yanatumika mara kwa mara. Hivi sasa Kichina ni moja ya lugha za kimataifa zinazotumiwa na watu wengi.

Watu wa kabila la Han wanapenda kula chakula cha nafaka, nyama na mboga. Tangu zamani sana, watu wa kabila la Han wamekuwa na desturi ya kula mara tatu kila siku. Vyakula vya mchele na unga wa ngano ni aina muhimu kwa wa-Han. Zaidi ya hayo, nafaka nyingine kama vile mahindi, mtama na viazi pia hutumiwa na wa-han katika sehemu tofauti. Kutokana na mila na desturi mbalimbali, watu wa kabila la Han katika sehemu tofauti wanakula vyakula vyenye ladha tofauti, kwa mfano watu wa kusini wanapenda vyakula vyenye sukari, watu wa kaskazini wanapenda vyakula vyenye chumvi chumvi nyingi zaidi, watu wa mashariki wanapenda kula vyakula vyenye pilipili na watu wa magharibi wanapenda vyakula vya tindikali. Hivi sasa, China ina aina nane kuu za vitoweo vyenye ladha tofauti.

Pombe na chai ni vinywaji viwili vikuu vya kabila la Han. China ni maskani ya chai, pia ni moja ya nchi zilizovumbua ufundi wa kutengeneza pombe mapema zaidi duniani, utamaduni wa pombe na chai wa China ni wenye historia ndefu. Licha ya pombe na chai, vinywaji vilivyotengenezwa na matunda pia vinapendwa sana na watu wa Han.

Watu wa Han wana sikukuu nyingi, sikukuu ya spring ya mwaka mpya ni sikukuu muhimu kabisa kwa kabila la Han. Zaidi ya hayo, sikukuu nyingine muhimu ni kama sikukuu ya taa (lantern festival) katika tarehe 15 Januari ya mwaka wa kijadi, siku ya Qingming ya kusafisha makaburi (Tomb-sweeping Day) ya tarehe 5 Aprili, sikukuu ya "dragon boat festival" ya tarehe 5 Mei na sikukuu ya "mid-autumn festiva" ya tarehe 15 Agosti, sikukuu hizo huwekwa katika kalenda ya kichina.

Wazhuang

Kabila la Zhuang ni kabila lenye idadi kubwa zaidi la watu kulingana na makabila madogo madogo mengine nchini China. Watu wa kabila la Zhuang wanaishi katika mkoa unaojiendesha wa kabila la Zhuang wa Guangxi, kusini mwa China, wanatumia lugha ya kizhuang, ambayo ni lahaja ya mfumo wa lugha wa Han-Tibet. Watu wa Zhuang ni wenyeji wa kusini mwa China, wana historia ndefu. Zaidi ya miaka elfu makumi iliyopita, wahenga wa Zhuang waliishi katika sehemu hiyo. Mkoa unaojiendesha wa kabila la Zhuang wa Guangxi ulianzishwa mwaka 1958.

Watu wa kabila la Zhuang wanajishughulisha na kilimo, hasa kilimo cha mpunga na mahindi. Watu wa Zhuang wanapenda kuimba, hivyo maskani ya kabila la Zhuang husifiwa kuwa "bahari ya nyimbo". Nguo za tarizi ni sanaa za mikono za kijadi za watu wa Zhuang. Watu wa Zhuang zamani walikuwa waumini wa dini ya kiasili ambao waliabudu maumbile na miungu wengi. Baada ya enzi ya Tang na Song, dini za Buddha na Tao zilienezwa hadi sehemu walikoishi watu wa Zhuang. Katika enzi ya hivi karibuni, dini ya kikristo pia zimeingizwa katika sehemu ya Zhuang, lakini haina athari kubwa.

Kabila la Man

Watu wa kabila la Man wanaishi kote nchini China, lakini wengi wao wanaishi katika mkoa wa Liaoning, kaskazini mashariki ya China. Watu wa kabila la Man walizungumza Kiman, ni lugha ya mfumo wa Altai. Baada ya kuishi pamoja na watu wahan, hivi sasa watu wengi wa Man wanatumia Kichina, ni wazee wachache tu wanaoishi katika vijiji vya pembezoni wanaweza kuzungumza lugha ya Kiman. Watu wa Man waliwahi kuamini dini ya Shaman yenye miungu wengi. Kabila la Man lina historia ya miaka zaidi ya 2000. Wahenga wao siku zote waliishi katika sehemu ya mtiririko wa kati na chini wa mto Heilongjiang na mtiririko wa mto Wusuli, kaskazini ya mlima wa Changbaishan, kaskazini mashariki mwa China. Katika karne ya 12, kabila la Man lililoitwa "Nuzhen", lilianzisha enzi ya Jin. Mwaka 1583 Nuerhachi aliunganisha makundi mbalimbali ya "Nuzhen", kuanzisha mfumo wa "Bendera Nane" za kabila la Man, na kuanzisha lugha ya Kiman, na kulipa kabila hilo jina la "Manzhou" mwaka 1635. Mwaka 1636, Nuerhachi akawa mfalme, na kuanzisha enzi ya Qing. Mwaka 1644, jeshi la enzi ya Qing lilisonga kusini na kuiangusha enzi ya Ming. Enzi ya Qing ilikuwa enzi kifalme ya mwisho ya ya China iliyo chini ya utawala wa serikali kuu. Baada ya mapinduzi ya Xinhai, kabila hilo lilianza kuitwa rasmi kuwa kabila la Man. Watu wa Man walitoa mchango mkubwa kwa umoja, upanuaji wa ardhi na maendeleo ya uchumi na utamaduni wa China.

Kabila la Hui

Kabila la Hui lina idadi ya watu zaidi ya milioni 9.8, wengi wao wanaishi katika mkoa unaojiendesha wa kabila la Hui wa Ningxia, kaskazini magharibi mwa China. Baadhi yao wanasambaa katika sehemu mbalimbali, ni kabila dogo linaloenea katika sehemu nyingi sana za China. Watu wa Hui wameishi pamoja na watu wa Han kwa kipindi kirefu, hivyo wengi wao wanazungumza lugha ya kihan, yaani Kichina. Watu wa Hui wanaoishi pamoja na watu wa makabila mengine madogo pia wanaweza kuzungumza lugha za makabila hayo. Baadhi ya watu wa Hui wanafahamu Kiarabu na Kiajemi. Tokea karne ya 7, wafanyabiashara wa kiarabu na kiajemi walikuja China, na kukaa katika miji ya Guangzhou, Quanzhou na mingine iliyoko pwani ya kusini mashariki mwa China, baada ya karne kadhaa, kikundi hicho cha watu hatua kwa hatua kimekuwa sehemu ya kabila la Hui. Mwanzoni mwa karne ya 13, watu wa Asia ya kati, waajemi na waarabu waliolazimishwa kuhamia sehemu ya kaskazini magharibi mwa China kutokana na vita nchini kwao waliishi pamoja na watu wa kabila la Han, Uigur na Mongolia kwa njia ya ndoa na dini, na kuunda kabila la Hui. Watu wa Hui ni waumini wa dini ya kiislamu, misikiti ilijengwa katika miji, vitongoji na vijiji vyote ambako wanaishi wahui. Watu wa Hui wana desturi maalum ya chakula na vinywaji, mikahawa na maduka ya chakula yanayowahudumia watu wa Hui yapo katika sehemu mbalimbali nchini kote. Watu wa Hui wana kiwango cha juu cha uchumi na utamaduni, na wametoa mchango mkubwa katika maendeleo ya historia ya China.

Kabila la Miao

Kabila la Miao lina idadi ya watu milioni 8.94, wengi wao wanaishi katika mikoa ya Guizhou, Yunnan, Sichuan, Guangxi, Hunan, Hubei na Guangdong. Kabila la Miao linatumia Kimiao, ni lugha ya mfumo wa Han-Tibet. Zamani kabila la Miao halikuwa na herufi za maandiko za lugha yao. Mwaka 1956, lilifanya mageuzi kwa lahaja nne na tutunga herufi za lugha yao kwa hahaja ya kilatin. Miao ni moja ya makabila yenye historia ndefu nchini China, kuna maandishi kuhusu kabila hilo kwenye vitabu vya historia vilivyochapishwa miaka zaidi ya 4000 iliyopita. Kwa mujibu wa maandishi hayo, mfalme wa "Huang" na mfalme wa "Yan" walianzisha vita dhidi ya "Chi You" ambaye alikuwa mhenga wa watu wa Miao. Kutokana na vita, njaa, magonjwa na ongezeko kubwa la idadi ya watu na kuachishwa kilimo mashamba yao, watu wa Miao walikuwa wakihamahama, na kusambaa katika sehemu nyingi kwa hivyo kuna tofauti kubwa kati ya vikundi mbalimbali vya watu wa Miao katika lahaja, mavazi, mapambo ya kichwani pamoja na mila na desturi. Watu wa Miao wanaoishi sehemu mbalimbali wanajiita kwa majina tofauti ya kikabila kutokana na umaalum wao wa mavazi kama vile "wamiao wa sketi ndefu", "wamiao wa sketi fupi", "wamiao wekundu" na "wamiao weusi". Watu wengi wa Miao ni wanaamini a dini ya kiasili ambayo kila kitu kina roho yake. Watu wa Miao wanalima mpunga na mahindi kwa wingi, pia wanalima mimea ya kiuchumi kama vile miti ya "tung-tree" na mboga wa "cole" na miti shamba ya aina mbalimbali.

Kabila la Yi

Kabila la Yi lina idadi ya watu zaidi ya milioni 7.7, ambao wengi wanaishi katika mikoa minne ya Yunnan, Sichuan, Guizhou na Guangxi kusini magharibi mwa China. Wanatumia lugha ya Kiyi, ni mfumo wa "Han-Tibet", wanaoishi pamoja na watu wa Han wanajua Kichina. Kabila la Yi ni kabila lenye idadi kubwa ya watu na historia ndefu, watu wake wanaenea katika sehemu nyingi. Zaidi ya miaka 2000 iliyopita, makundi ya kabila la Di, Qiang yalioishi katika sehemu ya kaskazini mwa China yalihamia kusini na kujiunga na wenyeji wa huko na kuunda kabila jipya la Yi. Kabila la Yi ulishikilia mfumo wa utumwa kwa kipindi kirefu. Baada ya kuasisiwa kwa China mpya mwaka 1949, mfumo wa utumwa katika jamii ya Yi ulitoweka hatua kwa hatua baada ya mageuzi ya kidemokrasia. Watu wa Yi waliamini miungu wengi, na dini ya Tao. Mwishoni mwa karne ya 19, dini ya kikristo ilienea hadi katika sehemu walikoishi, lakini wakristo ni wachache.

Kabila la Mongolia

Kabila la Mongolia lina idadi ya watu zaidi ya milioni 5.8, wanaishi katika mkoa unaojiendesha wa kabila la Mongolia ya ndani, na wilaya zinazojiendesha za kabila la Mongolia katika mikoa ya Xinjiang, Qinghai, Gansu, Heilongjiang, Jilin na Liaoning. Wanazungumza Kimongolia, ambacho ni mfumo wa lugha za Altai. Jina la "Mongolia" lilianzia katika enzi ya Tang, wakati ule, lilikuwa moja ya makundi mengi ya Mongolia ya sasa. Chanzo cha kundi hilo lilikuwa katika sehemu ya ukanda wa mashariki wa mto Erguna, baadaye lilihamia sehemu ya magharibi. Makundi mbalimbali ya Mongolia yalinyang'anyana watu, mifugo na mali, na kupigana vita bila kusita. Mwaka 1206, Tiemuzhen aliteuliwa kuwa kiongozi wa kundi la Mongolia, ambaye alipewa jina la mfalme "Chengjisihan". Tokea hapo, nchi ya Mongolia iliasisiwa na kabila la Mongolia lenye nguvu, utulivu na maendeleo likatokea rasmi katika sehemu ya kaskazini ya China.. Baadaye "Chengjisihan" aliunganisha makundi mbalimbali ya Mongolia, kuunganisha China na kuunda enzi ya Yuan. Watu wa Mongolia ni waumini wa dini ya Lama. Kabila la Mongolia limefanya mchango mkubwa katika sekta za siasa, jeshi, uchumi, sayansi na teknolojia, elimu ya falaki na hesabu, utamaduni , sanaa na matibabu.

Makabila Yenye Idadi ya Watu Wasiozidi Laki Moja

China ina makabila 20 madogo yenye idadi ya watu wasiozidi laki moja, makabila hayo ni Bulang, Tajik, Achang, Pumi, Ewenk, Nu, Jing, Kinuo, Deang, Baoan, Russia, Yugu, Uzbek, Menba, Elunchun, Dulong, Tataer, Hezhe, Gaoshan na Luoba.

Kabila la Luoba

Kabila la Luoba lina idadi ya watu takriban 3000, ni kabila lenye watu wachache kabisa nchini China. Wanaishi katika sehemu ya kusini mashariki ya mkoa unaojiendesha wa Tibet. Watu wa Luoba wanaoishi katika kaskazini ya wilaya ya Motuo wanazungumza Kitibet, wengine wanazungumza Kiluoba. Kiluoba ni lugha ya mfumo wa Hgan-Tibet, kuna tofauti kati ya lahaja za waluoba wanaoishi katika sehemu tofauti. Neno la Luoba linaasilia lugha ya Kitibet, maana yake ni "watu wa kusini". Kabla ya kuasisiwa kwa China mpya mwaka 1949, watu wa Luoba bado walirekodi mambo kwa kuchonga mbao au kufunga kamba, hawakuwa na maandishi, ni watu wachache tu waliojua Kitibet. Baada ya kuasisiwa kwa China mpya, watu wa Luoba walipewa haki ya usawa na makabila mengine. Chini ya msaada wa serikali na makabila mengine, wameanzisha maisha mapya kwa njia ya kisiasa uzalishaji mali, na kupata maendeleo ya kiuchumi na kiutamaduni. Waluoba wengi ni waumini wa dini ya kiasili.

Kabila la Dulong

Kabila la Dulong lina idadi ya watu zaidi ya 7400, wanaishi katika bonde la mto Dulong, wilaya inayojiendesha ya kabila la Dulong na kabila la Nu mkoani Yunnan. Wanazungumza Kidulong, lugha ya mfumo wa Han-Tibet, lakini haina herufi za maandishi. Wadulong wanaamini kuwa kila kitu kina roho, na kuabudu vitu vya kimaumbile. Mwanzoni kabila la Dulong liliitwa "Qiao". Katika enzi ya Ming na Qing liliitwa "Qiu" au "Qu". Baada ya kuasisiwa kwa China mpya, lilianza kuitwa "Dulong" kutokana na matakwa yao wenywe. Zamani, watu wa Dulong walitumia vifaa duni vya kiasili katika uzalishaji wa kilimo, kukusanya matunda na kuvua samaki. Baada ya kuasisiwa kwa China mpya mwaka 1949, wadulong walibadili hali hiyo duni ya uzalishaji mali. Watu wa Dulong ni wachapa kazi, wakarimu na wenye moyo wa kirafiki , na wanapenda kuwasaidia wengine wenye dhiki. Katika shughuli za uwindaji, mawindo hugawanyika kwa washirika wote. Watu wa Dulong ni watu wenye uaminifu na kufuata ahadi na maadili.

Kabila la Kinuo

Kabila la Kinuo lina idadi ya watu zaidi ya elfu 20, wanaishi kwenye mlima mrefu ulioko katika wilaya ya Xishuangbanna ya mkoa wa Yunnan, kusini magharibi mwa China. Wanazungumza Kikinuo, ambacho ni lugha ya mfumo wa Han-Tibet, lugha hiyo haina herufi za maandishi. Watu wa Kinuo zamani waliamini kuwa, kila kitu kina roho, na kuabudu wahenga. Hakuna maandishi kuhusu chanzo cha kabila la Kinuo. Watu wa Kinuo wanamwabudu Zhu Geliang, inasemekana kuwa, walikuwa sehemu ya askari wa jeshi la Zhu Geliang, walihamia kutoka kaskazini wakati lilipopiga vita kusini. Baada ya kuasisiwa kwa China mpya, wakinuo waliingia katika jamii ya ujamaa moja kwa moja kutoka jamii ya asili, na kubadili kabisa hali duni ya uzalishaji wa kilimo, kurekodi mambo kwa kuchonga kwenye mianzi, kufanya biashara ya kiasili ya kubadilishana vitu kwa vitu na kutibu magonjwa kwa kutoa sadaka. Hivi sasa kabila la Kinuo limekuwa na makada, madaktari, wafanyabiashara na wafundi wa kilimo.

Kabila la Elunchun

Kabila la Elunchun lina idadi ya watu zaidi ya 8000, wanaishi katika sehemu ya milima ya Xinanling mpakani mwa mkoa unaojiendesha wa Mongolia ya ndani na mkoa wa Heilongjiang. Katika tarafa ya Hulunber ya mkoa wa Mongolia imeanzishwa wilaya inayojiendesha ya kabila la Elunchun. Watu wa Elunchun wanazungumza Kielunchun, ni lugha ya mfumo wa Altai, ambayo haina herufi za maandiko, wote wanatumia lugha ya kihan, yaani Kichina. Maana ya "Elunchun" ni watu wanaoishi mlimani. Watu wa Elunchun zamani waliishi maisha kwa kuwinda wanyama, kuchuma matunda na kuvua samaki. Karibu wanaume wote ni wapanda farasi na wapiga mshale hodari, wanafahamu sana desturi na utaratibu wa maisha wa wanyama wa aina mbalimbali, wana uzoefu mwingi wa uwindaji. Hadi miaka ya 40 ya karne ya 20, walikuwa bado ni kabila la kuhamahama na kuwinda, mawindo hugawanyika kwa wastani, hata wazee, wadhaifu, na walemavu. Baada ya kuasisiwa kwa China mpya, watu wa Elunchun waliingia katika jamii ya ujamaa moja kwa moja. Hivi sasa wameacha maisha ya kuhamahama na uwindaji, na kujenga makazi, wakiwa kama walinzi wa misitu na wanyamapori. Watu wa Elunchun ni watu wenye akili na busara, wanaweza kutengeneza sanaa za mikono zenye nakshi nyororo kwa kutumia maganda ya miti ya Birch, kama vile nguo, viatu, sanduku, vikapu, mapipa, hata mashua nyepesi. Watu wa Elunchun ni waumini wa dini ya Shaman, wanaabudu wahenga na vitu vya kimaumbile,wanaamini kuwa kila kitu kina roho.

Kabila la Tataer

Kabila la Tataer lina watu karibu 5000, wanaoishi katika mkoa unaojiendesha wa kabila la Uigur wa Xinjiang, wengi wanaishi katika miji ya Yining, Tacheng na Urumqi. Wana lugha yao ya Kitataer, ni lugha ya mfumo wa Altai. Licha ya wazee, watataer wengi huzungumza lugha ya Kikhazak au Kiuigur. Kabila la Tataer lina maandiko ya herufi za kiarabu, lakini kutokana na kuishi pamoja na watu wa Khazak na Uigur, pia wanatumia maandiko ya makabila hayo mawili. Wa-tataer wengi ni waumini wa dini ya kiislamu. Mapema wakati wa enzi ya Tang, wa-tataer walitokana na kabila la "Dadan" kutoka nchi ya Turki iliyoko kaskazini mwa China. Katika karne ya 13, watu wa Mongolia walipofanya vita vya kuvamia sehemu ya magharibi, watu wa Ulaya waliwaita wamongolia "Tataer". Kuanzia mwanzoni mwa karne ya 19, baadhi ya wa-tataer walihamia mkoani Xinjiang kutoka Russia. Baada ya vita kuu ya pili ya dunia, wa-tataer wengine waliendelea kuhamia mkoani Xinjiang na kuanzisha rasmi kabila la Tataer la China. Wa-tataer wanaishi vijijini hushughulikia ufugaji na wa-tataer wasomi hasa walimu wanaishi mijini na kutoa mchango mkubwa kwa elimu ya mkoa wa Xinjiang.

Sera ya Kikabila ya China

China ni nchi ya muungano yenye makabila mengi. Serikali ya China inatekeleza sera ya usawa, umoja na kusaidiana, kuheshimu na kulinda imani ya dini ya makabila madogo pamoja na mila na desturi zao.

Mfumo wa kujiendesha katika maeneo ya makabila madogo ni moja ya mifumo muhimu ya kisiasa nchini China. Hii inamaanisha kuwa, chini ya uongozi wa serikali kuu, inaweza kuanzisha mikoa au wilaya zinazojiendesha katika maeneo ya makabila madogo, kuweka ofisi za madaraka na kutekeleza madaraka ya kujiendesha katika mikoa au wilaya hizo. Serikali kuu inahakikisha kutekeleza sheria na sera za kitaifa kutokana na hali halisi ya kienyeji katika maeneo ya makabila madogo; kuwaandaa makada wengi, na wafundi wa aina mbalimbali; wakazi wa makabila mbalimbali wanaoishi katika sehemu zinazojiendesha kama wachina wengine wanajishughulisha na ujenzi wa kisasa wa kijamaa wa China, kuharakisha maendeleo ya uchumi wa kienyeji, na kukuza utamaduni na kujenga sehemu zinazojiendesha zenye umoja na usitawi wakiwa chini ya uongozi wa chama cha kikomunisti cha China.

Kutokana na uzoefu wa miongo kadhaa iliyopita, yaani chama cha kikomunisti cha China kikiwa kama chama tawala kimetunga sera mbalimbali kuhusu suala la kikabila kama zifuatazo:

Uundaji, ukuaji na utowekaji wa makabila ni mwendo mrefu wa kihistoria, suala la kikabila litakuwepo kwa kipindi kirefu.

Awamu ya ujamaa ni kipindi cha kustawi kwa pamoja kwa makabila mbalimbali, vipengele vya pamoja vya makabila mablimbali vimeongezeka, lakini umaalum na tofauti kati ya makabila bado yapo.

Suala la makabila ni sehemu moja ya masuala yote ya kijamii, na litatatuliwa hatua kwa hatua katika mwendo wa kutatua masuala yote ya kijamii, hivyo suala la kikabila la China la hivi sasa litatatuliwa hatua kwa hatua katika juhudi za pamoja za kujenga ujamaa.

Bila kujali idadi ya watu, historia ndefu au fupi na kiwango cha maendeleo, makabila yote yametoa mchango katika ustaarabu wa China, hivyo yanapaswa kupata haki ya usawa. Tunapaswa kuimarisha umoja wa makabila mbalimbali na kulinda muungano wa taifa.

Kuleta ongezeko la uchumi ni jukumu la kimsingi la awamu ya ujamaa, pia ni jukumu la kimsingi la kazi ya kikabila la China katika kipindi cha hivi sasa. Makabila mbalimbali yanatakiwa kusaidiana ili kuleta maendeleo na usitawi wa pamoja.

Kuanzisha sehemu zinazojiendesha katika eneo la makabila ni mchango mkubwa uliotolewa na Chama cha Kikomunisti cha China kwa nadharia ya kikabila ya Maxism, ni utaratibu wa kimsingi wa kutatua suala la kikabila nchini China.

Jambo muhimu linalotakiwa kufanywa katika kushughulikia vizuri mambo ya kikabila na kutatua suala la kikabila ni kuwaandaa makada wengi wa makabila madogo wenye akili na maadili.

Suala la makabila hufungamana na suala la kidini, hivyo inapaswa kutekeleza sera ya dini ya taifa kwa pande zote na kwa njia sahihi wakati wa kushughulikia masuala yote ya makabila.

Aidha, serikali ya China inaposhughulikia kuhimiza maendeleo ya eneo la makabila madogo katika sekta za uchumi, utamaduni na elimu, na kuinua hali ya maisha na utamaduni ya watu wa makabila madogo , inapaswa kuheshimu imani zao za dini, na kuhifadhi urithi wao wa kiutamaduni. Imefanya sensa, kukusanya data, kufanya utafiti na kuchapisha vitabu kuhusu urithi wa kiutamaduni na urithi wa kidini na sanaa za kienyeji za makabila mbalimbali. China imetenga fedha nyingi katika kukarabati mahekalu na majengo ya kidini yenye thamani ya kihistorai na kiutamaduni katika eneo la makabila madogo.

Kuandaa na Kuteua Makada wa makabila Madogo

Serikali ya China inatilia maanani sana kazi ya kuandaa makada wa makabila madogo. Idadi ya makada wa makabila madogo imeongezeka kwa kiwango kikubwa, na wameshika nyadhifa za uongozi katika ngazi tofauti. Hivi sasa nyadhifa za wenyekiti wa mikoa mitano inayojiendesha, na wakuu wa tarafa 30 na wilaya 119 zinazojiendesha ni zinachukuliwa na makada wa makabila madogo.

Watu wa makabila mbalimbali wanashiriki katika usimamizi wa mambo ya kisiasa na kijamii. Katika bunge la umma na baraza la halmashauri ya kisiasa ya China, makabila 56 yana wajumbe au wawakilishi wake, ambao wanachukua zaidi ya asilimia 10.


1 2 3 4 5 6