Naibu waziri Uingereza ajiuzulu kuhusu Picha za ngono
Naibu wa waziri mkuu wa Uingereza, Damian Green, ameachishwa kazi baada ya kubainika kuwa alikiuka kanuni za uwaziri.
Bwana Green ambaye alikuwa mshirika wa karibu wa Waziri mkuu Theresa May alibainika kuwa alitoa taarifa zisizo sahihi kuhusu picha za ngono zilizokutwa kwenye komputa yake ya ofisini.
Damian Green alikuwa anachunguzwa pia juu ya madai ya kutowaheshimu wanawake wanaharakati katika chama chake cha Conservative.
Hata hivyo kiongozi huyo amekanusha kuhusika na mashitaka yote yanaomkabili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |