Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw. Mike Pompeo amesema kama Korea Kaskazini ikiweza kutimiza kutokuwa na silaha za nyuklia, Marekani itaondoa vikwazo dhidi ya nchi hiyo na kuyaruhusu makampuni binafsi ya Marekani kuwekeza nchini humo.
Bw. Pompeo amesema hayo jana katika kipindi cha telivisheni cha Shirika la matangazo ya Columbia, pia amesema Marekani itaisaidia Korea Kaskazini kupata ustawi wa uchumi.
Aidha Bw. Pompeo alipohojiwa na waandishi wa habari wa Shirika la Fox News amesema hiyo inamaanisha kuwa makampuni binafsi ya Marekani yataisaidia Korea Kaskazini katika sekta za nishati, ujenzi wa miundombinu na kilimo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |