Russia imemaliza mazungumzo na India kuhusu kuiuzia nchi hiyo mfumo wa kuzuia makombora wa S-400, na makubaliano hayo yatasainiwa siku zijazo.
Vyombo vya habari nchini Russia vvimesema, makubaliano ya mauzo ya mfumo huo wenye thamani ya dola za Marekani bilioni 6 yatasainiwa wakati rais Vladmir Putin wa Russia atakapofanya ziara nchini India mwezi wa Oktoba.
Habari zinasema, pande hizo mbili zinaharakisha kufanya mazungumzo kuepuka tishio litakalotolewa na Marekani dhidi ya upande wowote unaofanya ushirikiano wa kijeshi na Russia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |