Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Marekani ya kutengeneza ndege, Boeing, Dave Calhoun amesema, kampuni hiyo itakamilisha utengenezaji wa ndege aina ya 747 mwaka 2022.
Bw. Calhoun pia amesema kiwango cha utengenezaji wa 767 na 747 hakitabadilika, na kwamba kampuni hiyo itaendelea kuunga mkono uendeshaji wa 747 katika siku za mbele. Pia amesema kutokana na athari ya muda mrefu ya COVID-19, kampuni hiyo itafanya marekebisho ikiwa ni pamoja na kupunguza kiwango cha utengenezaji wa ndege za matumizi ya kibiashara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |