• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Timu tano zamfuata Kagere Simba

    (GMT+08:00) 2020-09-17 16:08:03

    Wakala wa mchezaji Meddie Kagere wa Simba, Patrick Gakumba, amesema kuwa amepokea ofa tano za mteja wake huyo na kama hataendelea kupata nafasi ya kucheza ndani ya timu hiyo, basi itabidi ahame mara baada ya kumaliza mkataba wake. Kagere amekuwa akikosa nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza katika michezo miwili mfululizo ya ligi, huku kocha wa Simba Sven Vandenbroeck akionekana kumtumia zaidi mshambuliaji John Bocco. Gakumba amesema kuwa mteja wake huyo amebakisha mkataba wa mwaka mmoja hivyo kama ataendelea kutopata nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza itabidi aondoke ndani ya Simba kwani amepokea ofa nyingi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako