Kenya huenda ikaanza tena mauzo ya maembe katika soko la Umoja wa Ulaya (EU) mwezi ujao baada ya kipindi cha miaka mitano.
Mkurugenzi wa bidhaa za kilimo nchini humo humo Benjamin Tito amesema, kwamba Kenya ilikuwa imewekewa marufuku kuuza maembe Ulaya kutokana na uwepo wa wadudu.
Amesema sasa Kenya imethibiti wadudu hao kupitia uundaji wa maeneo yasiyokuwa na wadudu katika maeneo yanayokuza maembe.
Masoko ya maembe ya Kenya huko Ulaya ni pamoja na nchini Uingereza na Ufaransa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |