Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imetangaza kumalizika kwa janga la Ebola, baada ya mlipuko wa ugonjwa huo miezi mitano iliyopita kusababisha vifo vya watu 55.
Waziri wa Afya nchini humo Eteni Longondo amesema, mlipuko huo wa 11 uliotokea kwenye Mkoa wa Ikweta umemalizika, ingawa bado kuna hatari ya kutokea tena.
Mlipuko wa hivi karibuni wa Ebola ulitangazwa Juni Mosi katika mkoa wa Ikweta baada ya kesi za ugonjwa huo kugunduliwa katika mji mkuu wa mkoa huo, Mbandaka na kuenea kwenye mikoa mingine.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |