• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Lima-Rais Hu Jintao aondoka Lima na kuelekea Ugiriki

    (GMT+08:00) 2008-11-24 11:19:56
    Rais Hu Jintao wa China amemaliza ziara yake nchini Peru, na ameelekea Ugiriki kutoka Lima mji mkuu wa Peru alasiri ya tarehe 23 kwa saa za Lima.

    Rais Hu aliwasili Lima tarehe 19 mwezi huu na kufanya ziara nchini Peru. Wakati wa ziara yake hiyo, viongozi wa China na Peru wamefikia makubaliano kuhusu kuendeleza ushirikiano kwenye sekta mbalimbali, na kutangaza kuwa mazungumzo kuhusu mkataba wa biashara huria ya nchi hizo mbili yamekamilika kwa mafanikio, na nchi hizo mbili zimeanzisha rasmi uhusiano wa kiwenzi na kimkakati.

    Rais Hu pia alihudhuria mkutano wa 16 usio rasmi wa wakuu wa APEC huko Lima, ambapo amefafanua msimamo wa serikali ya China kuhusu masuala ya kukabiliana na msukosuko wa fedha duniani, kusukuma mbele usalama wa nafaka na nishati, na kuunga mkono mazungumzo ya Doha.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako