Kikundi kinachoundwa na waitalia 33 ambao wanatalii kwa magari yao tarehe 17 kiliingia mkoani Xinjiang kutoka mpaka wa Huoerguosi, kaskazini magharibi mwa Xinjiang. Hicho ni kikundi chenye watalii wengi zaidi wa nchi za nje kutembelea Xinjiang baada ya tukio la "Julai 5".
Imefahamika kuwa kikundi hicho kiliingia nchini China saa 7 alasiri ya tarehe 17 kutoka nchini Khazakstan, watalii hao 33 watatembelea miji ya Yinin, Shihezi na Urumqi, pia watatembelea Tulufan na Hami.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |