Waziri wa mambo ya nje wa Malaysia Bw. Anifah Aman, waziri wa mawasiliano wa nchi hiyo Ong Tee Keat na maofisa wengine wa Malaysia, maofisa wa ubalozi wa China nchini humo na wajumbe wa wachina wanaoishi nchini humo walikwenda uwanja wa ndege kumlaki rais Hu Jintao.
Alipowasili uwanja wa ndege Rais Hu Jintao ametoa hotuba ya maandishi akipongeza maendeleo ya uhusiano kati ya China na Malaysia. Amesema China na Malaysia ni nchi zinazoendelea zilizoko sehemu ya Asia na Pasifiki, zina maslahi mengi ya pamoja. Ameeleza matumaini kuwa ziara yake hiyo inaweza kuongeza maelewano na urafiki kati ya nchi hizo mbili, kuimarisha ushirikiano wa kunufaishana kati ya nchi hizo mbili na kusukuma mbele uhusiano na ushirikiano wa kimkakati kati ya nchi hizo mbili uinuke kwenye kiwango kipya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |