• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • barua 0710

    (GMT+08:00) 2012-07-18 16:24:16
    Barua ya kwanza inatoka kwa msikilizaji wetu Yaaqub Saidi wa S.L.P 792-50100 Kakamega Kenya anaanza kwa kusema nawapa mkono wa heri na fanaka watangazaji, viongozi na wafanyakazi wote wa idhaa ya Kiswahili ya CRI nikitaraji kuwa nyote mu wazima huku mkiendeleza shughuli za kutuhudumia kwa vipindi na matangazo.

    Zifuatazo ni sababu zinazonifanya niseme taifa la China ni bora kati ya mataifa mengi hapa ulimwenguni, sisi tunaishi katika nchi ambayo utamaduni wa kichina umeacha athari zake, nasi tunajivunia jambo hilo. China inastahiki kuungwa mkono na kushirikiana nayo kutokana na ushujaa wake wa kusimama kidete mbele ya siasa za magharibi katika wakati huu ambapo dunia inashuhudia ongezeko la joto. Katika kipindi cha muda mrefu China imeweza kupiga hatua kubwa na kuwa na nafasi muhimu katika nyanja zote na hilo wananchi wa China, Kenya na ulimwenguni kwa ujumla wanalijua vyema.

    Kwa mfano katika kipindi cha muda mrefu sasa China imefanikiwa kutuma satalait katika anga za juu jambo ambalo linaweza kufanywa na nchi chache tu duniani, aidha baada ya kupita miaka 30 imeweza kulitilia kasi sana suala la nyuklia ambayo nchi za magharibi zinageuza kuwa suala la kisiasa na kufanya kisingizio cha kutishia mataifa mengine, wakati ambapo Shirika la kimataifa la nishati ya Atomiki limeunga mkono mara nyingi shughuli za nyuklia za China likisema ni za amani na hazijaenda kinyume na sheria za kimataifa.

    Katika upande wa maendeleo ya viwanda China pia imewathibitishia walimwengu kuwa inaweza kujiletea maendeleo. Kwa kweli katika kipindi kirefu taifa la China limefungua miradi mbalimbali na kupata maendeleo makubwa katika mambo ya teknolojia ya kijeshi na sayansi. China pia imefanikiwa kuandaa mazingira ya kunawirisha maadili bora na hivi sasa vijana wanayajua vyema masuala ya kitaifa na kimataifa na wanajivunia kwa utamaduni wao wenye utajiri mkubwa. Mwisho nawaombea kila la heri watangazaji wafanyakazi na uongozi wote wa CRI. Ahsante sana.

    Kwanza tunapenda kukushukuru sana msikilizaji wetu Yaaqub Saidi kwa barua yako yenye maoni murua kabisa. Kwa kweli China hivi sasa imepiga hatua kubwa sana katika maendeleo ya sayansi na teknolojia, na hivi majuzi tu imerusha chombo cha anga ya juu cha Shenzhou no 9 ambacho kimebeba wanaanga watatu akiwemo mwanamke mmoja, hayo ni mafanikio makubwa kwa China, isitoshe imejaribu kuandika historia kuwa China nayo imekuwa miongoni mwa nchi zenye wanaanga wanawake, Ahsante sana.

    Na sasa ni barua ya Claude Magoye Kumalija wa S.L.P 1067 Kahama Shinyanga Tanzania anasema natumai mu wazima wafanyakazi wote wa CRI Idhaa ya Kiswahili, na mimi ni mzima na naendelea na ujenzi wa taifa langu la Tanzania pamoja na kufuatilia kila siku matangazo ya CRI na kuwaandikia barua mara kwa mara redio hii niipendayo ya CRI.

    Kabla ya yote natumia fursa hii kuwapongeza wafanyakazi na wananchi wote wa China kwa sikukuu ya mwaka mpya wa jadi wa China ambapo katika mwaka huu wa 2012 unawakilishwa na mnyama Dragoni. Baada ya hayo nachukua fursa hii kuipongeza CRI kwa kutuletea habari nyingi na nzuri katika kipindi kizima cha mwaka uliopita wa 2011 ambapo na katika mwaka huu pia tunaiomba CRI iendelee kufanya hivyohivyo.

    Mwisho naishukuru CRI kwa kunitumia bahasha, kadi za salamu pamoja na jarida la CRI la Daraja la Urafiki ambapo limerejea tena baada ya kulikosa kipindi cha muda wa miaka sita iliyopita. Ahsanteni sana uongozi mzima wa CRI kweli sisi wasikilizaji wenu mnatujali na kutupenda sana.

    Shukran za dhati msikilizaji wetu Claude Magoye Kumalija kwa barua yako, kama lilivyo lengo la CRI hususan idhaa ya Kiswahili kwamba ni kuwaletea habari motomoto za dunia ambazo tunataraji kuwa zitawaridhisha na kuwaelimisha wasikilizaji wetu wote, hivyo usiwe na wasiwasi kwani mwaka huu tutajitahidi kufanya vizuri zaidi kuliko mwaka jana asante sana.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako